HUYU NDIYE KOCHA MPYA YANGA, ANATUA DAR JUMAPILI

HUYU NDIYE KOCHA MPYA YANGA, ANATUA DAR JUMAPILI


KOCHA mpya wa Yanga kijana mwenye umri wa miaka 39, Tom Saintfiet (pichani kushoto) anatarajiwa kuwasili Dar es Salaam Jumapili, tayari kuanza kazi.
Habari za uhakika kutoka Yanga, zimesema kwamba huyo ndiye atarithi mikoba ya Mserbia Kosta Papic, baada ya jaribio la kumpata kocha wa zamani wa Taifa Stars, Marcio Maximo kugonga mwamba.
“Atawasili Jumapili, hapa ndio tunashughulikia tiketi yake,”alisema mtoa wa habari wetu kutoka Yanga, 

MATAJI ALIYOTWAA

  • 2009 Mshindi wa kocha bora wa mwaka  (Namibia)
  • 2008 Kocha bora wa mwaka  (Namibia)
  • 2008-2010 Tuzo maalum kuifikisha Namibia nafasi ya 30 viwango vya FIFA
  • 2008+2009 Robo Fainali Kombe la  COSAFA  (Afrika Kusini)
  • 2005 Kufuzu Nusu Fainali Kombe la NFV(Ujerumani)
  • 2005 Kutwaa Kombe la McDonald (Ujerumani)
  • 2004 Nafasi ya Tatu (Medali ya Shaba) Michauno ya U17 Asia 2004 nchinu Japan, Septemba 2004. Kufuzu Kombe la Dunia 2005 U-17 
  • 2002 Mshindi wa pili katika Ligi  (Visiwa vya Faroe)
 

Post a Comment

أحدث أقدم