KENNETH ASAMOAH ATEMWA YANGA - KULIPWA FIDIA

KENNETH ASAMOAH ATEMWA YANGA - KULIPWA FIDIA

Hatimaye mshambuliaji wa Yanga kutoka Ghana Kenneth Asamoah ametemwa na klabu hiyo baada ya kuitumikia kwa takribani msimu mmoja tu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Yanga, Asamoah amefikia makubaliano na Yanga kwa kulipwa fidia ya kuvunjiwa mkataba wake aliousaini msimu uliopita.

Kenneth Asamoah anaondoka Yanga huku akiwaachia wapenzi wa klabu hiyo kumbukumbu ya goli zuri la kichwa alilowafunga Simba kwenye fainali ya kombe la Kagame mwaka jana kwenye uwanja wa Taifa.

Post a Comment

Previous Post Next Post