Ccm yakipiga jeki kituo cha watoto yatima fema matamba wilayani makete

 Watoto yatima waliopo kwenye kituo cha Fema Matamba.
 Katibu wa CCM wilaya ya Makete Miraji Mtaturu akiongea na watoto na walezi wa kituo cha watoto yatima FEMA Matamba.
 Katibu wa CCM wilaya ya Makete Miraji Mtaturu akisalimiana na watoto yatima wa kituo cha Fema Matamba.
 Katibu akimpa mlezi wa watoto hao misaada hiyo
 Sehemu ya misaada iliyotolewa na chama hicho
Muonekano wa kituo cha watoto yatima FEMA Matamba.
==========
Jamii nchini imetakiwa kujenga desturi ya kusaidia wasiojiweza hasa watoto waishio katika mazingira hatarishi na wanaolelewa katika vituo vya watoto yatima kwa kuwa hawakupenda kuishi maisha wanayoishi ya kukosa wazazi

Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na Katibu wa CCM wilaya ya Makete Miraji Mtaturu wakati akikabidhi vitu mbalimbali vilivyotolewa na chama hicho vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 60,000 kwa ajili ya watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha FEMA Matamba kilichopo chini ya KKKT kilichopo kata ya Matamba wilaya ya Makete mkoani Njombe

Mtaturu amesema wao kama chama wameguswa na namna watoto hao wanavyoishi katika kituo hicho kuwa wanahitaji misaada ya kila namna kutoka kwa wanamakete na ndio maana wamefikia hatua hiyo ambayo wanaimani itaungwa mkono na watu wengine

"hawa watoto ni wetu na hakuna anayeweza kuja kutusaidia kuwalea kwa uchungu kama sisi wenyewe, sisi kama chama cha mapinduzi wilaya ya makete tumeonesha mfano kwa hiki kidogo tulichokileta tunaomba na wengine wawasaidie watoto hawa" alisema Mtaturu

Kwa upande wake askofu Job Mbwilo ameshukuru kwa msaada huo uliotolewa na CCM wilaya ya Makete na kusema anaimani kuwa wapo wengine watakaojitokeza kuwaunga mkono hasa ukizingatia kituo hicho hakina mradi unaokiwezesha kupata fedha zaidi ya kutegemea misaada kwa wajerumani pamoja na wadau wengie wanaoguswa kuwasaidia kutoka ndani na nje ya nchi
 
Chama hicho kimetoa sukari, sabuni pamoja na biskuti kwa ajili ya watoto hao

Post a Comment

Previous Post Next Post