WEMA ANASWA AKIKATA MAUNO

Na Mwandishi Wetu
MADAM, Wema Sepetu ameonesha upande wa pili wa maisha yake baada ya kunaswa akikata mauno mwanzo mwisho.
Kwa mujibu wa mtandao mmoja wa Kibongo, Madam alifi ka na kampani yake katika Ukumbi wa Thai Village, Masaki jijini Dar hivi karibuni na ndipo ‘mashetani’ yalipompanda baada ya kusikia sebene lililokuwa likiporomoshwa na Bendi ya Skylight.
Wema akiwa na kampani yake wakionekana kukolea kwa kilevi, waliinuka na kuanza kushindana kucheza huku Wema akijiweka ziro distance na mmoja wa wanamuziki wa bendi hiyo na kuanza kumkatikia.

Post a Comment

Previous Post Next Post