Benki ya Covenant yatoa maabasi na bajaji kwa wajasiriamali


Mwenyekiti wa  Benki ya  Covenant  Balozi Salome Sijaona  akimkabidhi  mratibu wa uhamasishaji wa vikundi vya Wilaya ya Temeke Bi.Tukae Kondo ufunguo wa pikipiki baada ya kuwapatia mikopo wajasiliamali mbalimbali.Benki hiyo kwa kushirikiana na umoja wa wafanyakazi wasio katika sekta rasmi imewawezesha wajasiriamali wadogo nchini kwa kuwapatia mikopo na mitaji. Hafla hiyo imefanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Covenat bank Sabetha Mwambenja.
 Mkurugenzi Mtendaji wa  benki ya Covenat  Sabetha Mwambenja, akiwasisitizia  jambo juu  ya kurejesha mikopo baadhi ya wajasiriamali waliopata mikopo  ya pikipiki  iliyotolewa na Benki hiyo kwa kushirikiana na umoja wa wafanyakazi wasio katika sekta rasmi wamewawezesha wajasilia mali wadogo nchini kwa kuwapatia mikopo . Hafla hiyo imefanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es salaam. Kushoto anayeshuhudia ni Mwenyekiti wa bodi wa benki hiyo Balozi Salome Sijaona
Mwenyekiti wa  Benki ya  Covenant  Balozi Salome Sijaona  akimkabidhi  Mwenyekiti wa Kikundi cha Mshikamano cha  Yombo Vituka cha jijini Dar es Salaam,Charles Rweyemamu  ufunguo wa gari aina ya basi lenye thamani ya shilingi Milioni 45 .Benki hiyo kwa kushirikiana na umoja wa wafanyakazi wasio katika sekta rasmi wamewawezesha wajasiriamali wadogo nchini kwa kuwapatia mikopo. Hafla hiyo imefanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Covenat bank Sabetha Mwambenja.
*********
Benki ya Covenant kwa kushirikiana na Umoja wa wafanyakazi wasio katika sekta rasmi katika kuwawezesha wajasiriamali wadogo nchini wamewawezeha wajasiriamali zaidi ya 60 kujikwamua kimaisha kwa kuwapatia mikopo ya mitaji ambayo imejumuisha, Basi za abiria, Pikipiki za miguu mitatu maarufu kama bajaji pamoja na pikipiki Ushirikiano utakaowezesha zaidi ya wajasiriamali wadogo takribani milioni 6.8 ambao wote ni wanachama wa chama hicho nchini.

Akizunumza wakati wa makabidhiano hayo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo Balozi.Salome Sijaona  amesema kuwa benki yake imeendelea kuwapa kipaumbele watu wote wa chini ambao hawajafikiwa na huduma za kibenki na sasa wamewekeza zaidi katika kuwawezesha wajasiriamali hao kwa kuwapatia mitaji endelevu itakayo wawezesha kuingiza kuwaingizia kipato moja kwa moja.

“Benki yetu iko katika msitari wa mbele kuwawezesha Watanzania na wajasiriamali ambao hawako katika sekta rasmi na hawajafikiwa na huduma za kibenki, katika kuhakikisha tunafikia malengo haya, tumeweza kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha tunafikisha huduma zetu kwa watu wote,” alisema Mwenyekiti huyo na kuongeza kuwa.

Post a Comment

Previous Post Next Post