IKULU:Rais Jakaya Kikwete Awasili Brazil

Rais
Jakaya Mrisho kikwete akiongea na Msaidizi Mwandamizi wa Rais
(Diplomasia) Balozi Liberata Mulamula baada ya mkutano wa maandalizi ya
ziara yake ya siku tano nchini Brazil Jumapili Aprili 15, 2012 katika
hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo. katikati ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi
Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman.

Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono
mwandishi mwandamizi wa Habari
Leo na Daily News,
Bw Joseph Lugendo, alipokuwa analakiwa baada ya
kuwasilii Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya
Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na
kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji
(TIC) Bw Raymond Mbilinyi,
baada ya kuwasili
Jumapili Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli
jijini Sao
Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi
nchini
humo

Mke
wa Rais Mama Salma kikwete akipokea shada la maua mara baada ya yeye
na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwasili Jumapili Aprili 15, 2012 katika
hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil, tayari kwa ziara ya siku
tano ya kikazi nchini humo. Kulia kwake ni Rais Kikwete na nyuma kulia
ni Waziri wa kazi
na
Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa
Zanzibar Mh Haroun Ali
Suleiman na mwenye mwani
ni Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Mh
Francis
Malambugi.

Rais
Jakaya Mrisho kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili Jumapili
Aprili 15, 2012 katika hoteli ya Tivoli jijini Sao Paulo, Brazil,
tayari kwa ziara ya siku tano ya kikazi nchini humo. Kulia ni Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa
Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman.Picha na IKULU
--

Rais Jakaya Mrisho kikwete amewasili Brazil Jumapili
Aprili 15, 2012 kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku
tano.Katika
ziara hiyo Rais Kikwete anatarajia
kukutana na kufanya mazungumzo na
mwenyeji wake
Rais Dilma Varna Rousseff wa Brazil na Rais
mstasafu wa
nchi hiyo Mheshimiwa Inacio da Silva
Lula na viongozi waandamizi wa nchi
hiyo.
Katika
ziara hiyo, Rais Kikwete atahudhuria mkutano
wa mwaka wa wakuu wa nchi
zinazoshiriki katika
Mpango wa Ubia wa Uwazi Serikalini (Open
Government Partnership-OGP) utakaofanyika
mjini Brasilia chini ya
Uenyekiti wa Rais Rousseff na
kuhudhuriwa na wajumbe wapatao mia nne
(400)
kutoka serikalini, Asasi zisizo za kiserikali, Sekta
binafsi
pamoja na Mashirika ya Kimataifa.
Ubia
wa Uwazi Serikalini au kwa kifupi OGP, ni mpango
uliozinduliwa Septemba 2011 mjini New York, Marekani kwa lengo la
kuwapa wananchi nafasi ya kushiriki katika kuamua mambo yanayowahusu,
kupitia vyama visivyo vya Kiserikali na vya Kijamii.
Ubia
huu unashirikisha kwa usawa wawakilishi wa serikali kwa upande mmoja
na wawakilishi wa Asasi zisizo za Kiserikali za Kijamii kwa upande
mwingine. Nchi ya Brazil kwa kushirikiana na Marekani imekuwa mstari wa
mbele katika kusukuma ubia huu.
Rais
Kikwete anatarajiwa kuhutubia mkutano huo tarehe 17 Aprili, asubuhi
mara tu baada ya hotuba ya ufunguzi itakayotolewa na Mwenyekiti wa
mkutano huo Rais Dilma Rousseff wa Brazil, ambapo ataelezea maendeleo
iliyofikia katika kuandaa mpango kazi wa kutekeleza ahadi ya kuongeza
uwazi kama ilivyokubaliwa katika kikao kilichofanyika Disemba 2011.Rais
Kikwete anatarajiwa kurejea nchini tarehe 20 Aprili, 2012.
Post a Comment