Tusipodhibiti Ujinga Dhidi Ya Freemasons Taifa Litaangamia

Tusipodhibiti Ujinga Dhidi Ya Freemasons Taifa Litaangamia

Tusipodhibiti Ujinga Dhidi Ya Freemasons Taifa Litaangamia


Picha hii imepigwa posta Dar es salaam.Ni mhubiri anyejifanya anazungumza dhidi ya freemason,lakini nadhani anaimarisha ujinga kuhusu dudu hili

Wapo watakaoona nakazania jambo dogo,wanapaswa kutafakari tena.sasa kila kona ya nchi hii,watu wajinga kwa waerevu,wasomi na wasiosoma,wakuu wa dini na wengi wengine waimba wimbo wa freemasons,jamii inaaminishwa hiki ni kikundi(dini)? ya kishetani inayoweza kusababisha kichawi ajali ili freemason wanywe damu za watu,eti wanaweza kuwapa watu utajiri kishetani,eti wanatawala dini zote kubwa,eti viongozi wote na watu wote maarufu ni wanafreemason,eti majengo yote makubwa kama kanisa la mtakatifu Petro Roma,Msikiti mkuu wa Makka,makao makuu ya Anglicana Cantebury,Umoja wa Mataifa,Umoja wa Ulaya,Umoja wa Afrika,ikulu za nchi zote,mabenki,mahospitali yana nembo za utambulisho wa uanachama wa freemason.UJINGA JUU YA UJINGA.Eti wanatumia ishara,vidole viwili "V" ,namna wanavyokumbatiana nk. UJINGA JUU YA UJINGA.Haki ya nani tutakuja kuambiwa hata tendo la ndoa ni ufreemason!!! nani atabaki??
  Hatari ya wazi ni kuwa Ujinga huu unaosambaa kwa uzushi kwa wajinga kuwaambia wajinga wenzao hata wasomi wanaoamini ujinga huu ni wajinga vilevile kwa sababu inawezekana kusoma habari za kweli juu ya freemason na kuelewa,sasa ni vipi wasomi uchwara wanaamini mizungu.hatari nyingine ni shambulio la imani za kidini.dini zote kubwa zimehusishwa na freemason,oooh mara papa wa wakatoliki na maaskofu hawa na wale ni freemasos,ooh mara makka kwenye kaaba kuna ishara ya freemasons,UJINGA JUU YA UJINGA. Hatri nyingine na iliyonifanya kuandika hii tafakari ni imani potofu kuwa freemason wanafanya mtu awe tajiri,nilipoandika mara ya kwanza hapa siku za nyuma kuna waliodhani ninajua juu ya freemason,walinipigia simu na hasa vijana wakiniuliza namna ya kujinga ili watajirike,siku nyingi baadaye juzi nimekutana na rafiki yangu wa siku nyingi mhitimi wa chuo kikuu,na sasa ni mwalimu kwenye chuo kikuu kimoja nchini,na anataka kugombea ubunge mwaka 2015,akanieleza anavyopanga kupata pesa za uchaguzi huo kuwa anatafuta uwezekano wa kujiunga na freemason sasa ili kufikia 2015 awe ameshakuwa tajiri.naam atakuwa mbunge gani huyu? anaamini ushirikina,kupata fedha za miujiza,ama kweli waafrika tumelaaniwa(ikubaliwe kwa ajil ya makala haya?
   Mhubiri huyu wa posta anongea ujinga wake mchana kweupe,anataja watu majina baadhi yao viongozi wa dini na serikali na kuwahusiha na ibada za shetani,anaendelea bila kuulizwa.tunajenga taifa la namna gani? wapo watu na magazeti kama jambo leo na tazama yanasaidia kueneza ujinga huu,hakuna anyelinda wasomaji wa habari tanzania? TUMEKWISHA
Na Ludovick
0715 927100   ,,0753927100

Habari kwa hisani ya   :- Fredy njeje

Post a Comment

Previous Post Next Post