VIONGOZI WA DINI WAPIGWA MSASA KUHUSU SENSA YA WATU NA MAKAZI 2012



VIONGOZI WA DINI WAPIGWA MSASA KUHUSU SENSA YA WATU NA MAKAZI 2012


Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ramadhani
 Khijjah akizungumza na viongozi mbalimbali wa dini 
kuelezea umuhimu na ushiriki wao katika kufanikisha sensa 
ya watu na makazi itakayofanyika kitaifa mwezi Agosti 
mwaka huu  wakati wa mkutano wa viongozi wa dini 
unaoendelea  jijini Dar es salaam.  

Baadhi ya viongozi wa dini wanaoendelea na mkutano wao
 jijini Dar es salaam wakipitia vitabu na vipeperushi  vyenye 
jumbe mbalimbali  kuhusu zoezi la sensa ya watu na makazi
 litakalofanyika nchi nzima mwezi  Agosti mwaka huu  baada
ya wataalam kutoka  Ofisi ya Taifa ya Takwimu kutoa semina
fupi kuhusu ushiriki wa viongozi hao katika kufanikisha 
sensa hiyo .

Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini 

wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu mkuu wa Wizara ya
 Fedha na uchumi Ramadhani Khijjah alipokuwa 
akizungumzia umuhimu wa sensa ya watu na makazi  2012 
na namna serikali ilivyojipanga kukamilisha zoezi hilo kwa 
ufanisi.


Mkurugenzi mkuu ofisi ya taifa ya takwimu Dkt. Albina 
Chuwa akisisitiza jambo kuhusu sensa ya watu na makazi 
itakayofanyika mwaka huu wakati wa semina ya viongozi wa 
dini jijini Dar es salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ramadhani 
Khijjah (kushoto) akiandika maswali yaliyoulizwa na viongozi
 wa dini kuhusu namna serikali ilivyojipanga kukamilisha 
sensa ya watu na makazi  itakayofanyika mwezi Agosti 2012.
 Wengine ni mkurugenzi mkuu wa ofisi ya taifa ya takwimu 
Dkt. Albina Chuwa (katikati) na kamishna wa sensa Bi. 
Hajjat Amina Mrisho.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ramadhani 
Khijjah (kushoto) akizungumza jambo na mkurugenzi mkuu 
wa ofisi ya taifa ya takwimu Dkt. Albina Chuwa wakati wa 
mkutano wa mkutano wa viongozi wa dini unaoendelea jijini 
Dar es salaam. Ofisi ya taifa ya takwimu imekutana na 
viongozi hao kufuatia umuhimu na ushawishi wao katika 
jamii ili waweze kushiriki kikamilifu katika kufanikisha sensa
ya makazi itakayofanyika mwezi Agosti 2012. 
Picha na Aron Msigwa- MAELEZO.

Post a Comment

Previous Post Next Post