WACHANGIA MFUKO WA KUSAIDIA WENYE ULEMAVU WA NGOZI (ALBINO)
watu wenye ulemavu wa ngozi wakiingia katika viwanja vya Mnazi Mmoja kumalizia maandamano yao yaliyoanzia katika viwanja vya Leaders jana, maandamano hayo yaliandaliwa na Taasisi ya Badef kwa lengo la kuchangisha fedha za kusaidia albino nchini
Mbunge wa viti maalum Viti Maalum Mh.Shaimaar Kwegyr akisalimiana
na washiriki wa maandamano hayo mara baada ya kufika katika
viwanja vya Mnazi mmoja leo.
na washiriki wa maandamano hayo mara baada ya kufika katika
viwanja vya Mnazi mmoja leo.
Shilingi milioni mbili zimekusanywa katika Harambee ya kusaidia kampeni ya
kufanikisha maendeleo ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini iliyofanyika
leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Waliochangia fedha hizo ni Waziri wa Afya na Usatwi wa Jamii Mh.Dkt. Hadji
Mponda aliyetoa milioni moja,Meya wa Manispaa Kinondoni Ndg.Yusuph
Mwenda alitoa laki tano huku Mbunge wa Viti Maalum Mh.Shaimaar Kwegyr
akitoa laki tano.
Mponda aliyetoa milioni moja,Meya wa Manispaa Kinondoni Ndg.Yusuph
Mwenda alitoa laki tano huku Mbunge wa Viti Maalum Mh.Shaimaar Kwegyr
akitoa laki tano.
Akizungumza na watu waliojitokeza katika matembezi hayo Mwenyekiti wa
Taasisi inajishughulisha na maendeleo ya watu wenye ulemavu iitwayo Badef,
Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mh.Salum Barwany ambae Mbunge wa Lindi Mjini
alisema kuwa shilingi milioni 500 zinahitajika.
Taasisi inajishughulisha na maendeleo ya watu wenye ulemavu iitwayo Badef,
Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mh.Salum Barwany ambae Mbunge wa Lindi Mjini
alisema kuwa shilingi milioni 500 zinahitajika.
Mh.Barwany alisema kuwa walemavu wa ngozi wanakabiliwa na tatizo la
kansa ya ngozi ambayo inawashika kiurahisi zaidi kutokana na ngozi yao
hivyo fedha hizo zitasaidia kuwanunulia mahitaji muhimu watu hao.
kansa ya ngozi ambayo inawashika kiurahisi zaidi kutokana na ngozi yao
hivyo fedha hizo zitasaidia kuwanunulia mahitaji muhimu watu hao.
Alisema kuwa pia wanakabiliwa na tatizo la elimu kwa kuwa watu wenye
ulemavu wa ngozi wana tatizo la kuona mbali hali inayowafanya kushindwa
kuona vema darasani hivyo wanahitaji msaada maalum.
ulemavu wa ngozi wana tatizo la kuona mbali hali inayowafanya kushindwa
kuona vema darasani hivyo wanahitaji msaada maalum.
Alisema kuwa hizo ni moja kati ya changamoto ambazo jamii inatakiwa
kuwasaidia walemavu hao kukabiliana nazo ambapo ili kufanikisha hilo kuna
haja ya kufanya utafiti.
kuwasaidia walemavu hao kukabiliana nazo ambapo ili kufanikisha hilo kuna
haja ya kufanya utafiti.
Alisema kuwa fedha hizo zitasaidia kufanya utafiti wa kubaini namna ya
kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi katika nyanja za elimu, kijamii na
hata uchumi.
kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi katika nyanja za elimu, kijamii na
hata uchumi.
Pia Mh.Barwany alisema kuwa fedha hizo zitasaidia kuwasafirisha kiurahisi
albino ambao watakuwa na dalili za kansa ya ngozi ili kuwahi katika hospitali
za rufaa kwa ajili ya matibabu.
albino ambao watakuwa na dalili za kansa ya ngozi ili kuwahi katika hospitali
za rufaa kwa ajili ya matibabu.
“ Kwa sasa sisi walemavu wa ngozi tunahitaji milioni 500 ili angalu tuweze
kusimamia na kujipatia mahitaji yetu muhimu ya kiafya hapa nchini, hivyo
wanajamii tunaomba tusaidiane katika hilo tafadhali” alisema Barwany.
kusimamia na kujipatia mahitaji yetu muhimu ya kiafya hapa nchini, hivyo
wanajamii tunaomba tusaidiane katika hilo tafadhali” alisema Barwany.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo alitakiwa kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa
Jamii Mh.Dkt.Hadji Mponda ambae hakuwepo na hivyo aliwakilishwa na
Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda.
Jamii Mh.Dkt.Hadji Mponda ambae hakuwepo na hivyo aliwakilishwa na
Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda.
Maandamano yalianzia Viwanja vya Leaders na kumalizikia viwanja vya
Mnazi Mmoja.
Mnazi Mmoja.
Vilevile unaweza kuchangia kupitia: Mpesa Namba; 0769696999, Airtel Money Namba; 0688858535, TigoPesaNamba; 0655029595 au kwenye akaunti ya BADEF (CRDB Bank, Lumumba Branch Akaunti Na. 0150278228900).
Habari kwa hisani ya:- http://dj-sek.blogspot.com
Post a Comment