Hali bado ni tete Zanzibar

Kikosi
cha Kuzuwia Fujo FFU kikizunguka kikiwa kimejihami katika maeneo ya
Michenzani ambapo tayari jeshi la polisi limepiga marufuku mikusanyiko
yoyote Mjini hapa
WASIWASI mkubwa
umetanda kwa siku ya pili mfululizo katika mitaa ya miji ya Zanzibar
baada ya askari wa jeshi la polisi kupiga mabomu ya kutoa machozi ili
kuwatawanya wafuasi wa taasisi za kidini zinaozongozwa na Jumuiya ya
Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI).
Wafuasi hao ambao
walikusanyika katika makao makuu ya polisi mkoa wa mjini magharibi
Madema jumamosi jioni, kushindikiza kutolewa kwa viongozi wao
wanaoshikiliwa kituoni hapo.
Kamishna wa jeshi la
polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa aliwaambia waandishi wa habari kuwa
wafuasi hao wamefanya uharibifu mkubwa ikiwa pamoja na kuchoma moto
makanisa mawili na kwamba watu saba wanaotuhumiwa saba wamekamatwa na
jeshi hilo.
Akizungumzia kuhusu
hali hiyo ofisini kwake Ziwani Mjini Unguja Kamishna Mussa alisema
kwamba jeshi lake litaendelea kuwasaka na kuwatia mikononi wote
waliopanga fujo hizo pamoja na viongozi wote wa jumuiya ya Uamsho.
“Jumuiya ya Uamsho na
Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar ndio iliyohusika na kuwachochea vijana
kukusanyika na kufanya uharibifu ikiwemo kuchoma moto gari, kupanga mawe
barabarani na kufanya hujuma mbali mbali kinyume cha sheria.
Tutaendelea kuwasaka kwa gharama zote” alisema Mussa.
Kamishna alisema kwa
sasa mikusanyiko yote ya mihadhara ya kidini na vyama vya siasa lazima
ipate kibali cha polisi vyenginevyo jeshi lake litatumia nguvu za ziada
kutawanya mikusanyiko hiyo ili kulinda sheria za nchi, amani na utulivu.
Maeneo kadhaa na mji wa Zanzibar hasa
Kwa habari zaidi ingia hapa:- www.zanzibaryetu.wordpress.com
Post a Comment