Halmashauri za Wilaya Morogoro kukusanya zaidi ya Sh. Bil. 24

Zaidi ya shilingi bilioni 24 zinatarajiwa kukusanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013.
Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 1.23 ni kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri,\ ruzuku kutoka Serikali kuu ni shilingi bilioni 19.5 
na miradi ya maendeleo shilingi bilioni 4.8.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Eden Munisi na Mwenyekiti wa Halmashauri Bi Kibena Kingo wamesema hayo wakati wakitoa mapendekezo ya makadirio ya Bajeti ya mapato na matumizi ya kawaida, mishahara na miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2012/2013 katika kikao Baraza la Madiwani kilichofanyika wilayani humo.
Kiwango hicho cha Bajeti kimeongezeka kwa kiasi cha shilingi bilioni 3.1 sawa na asilimia 12.8 ikilinganishwa na shilingi bilioni 21.2 za bajeti iliyotarajiwa kukusanywa mwaka wa fedha 2011/2012.
Madiwani wameelezea kukerwa kwao na kitendo cha Halmashauri hiyo kupokea kiwango kidogo cha fedha kutoka serikalini kwa ajili ya matumizi ya kawaida tofauti na makisio na baadhi ya fedha za miradi ya maendeleo kutotolewa kabisa na hivyo kukwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post