MWENYEKITI
WA HALMASHAURI YA ILEJE BW. MOHAMED MWALA(mwenye joho jekundu)
AKISISITIZA JAMBO KATIKA KIKAO KILICHOKETI KUMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI
Madiwani
wa halmashauri ya wilaya ya Ileje wamemsimamisha kazi Mkurugenzi wa
halmashauri hiyo Bi. Sylivia Siriwa kwa madai ya kuhusika na hujuma na
ubadhirifu wa mali za halmashauri hiyo.
Hatua hiyo imefuatia tuhuma zilizoelekezwa kwake katika kikao cha baraza
la Madiwani kilichoketi kujadili jaribio la wizi wa fedha za
halmashauri zilizofanywa na watumishi wanne ambapo Mkurugenzi huyo
alishindwa kuwachukulia hatua za kisheria.
Akizungumza
katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ileje Bw. Mohamed Mwala
amesema kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya Baraza kujigeuza kamati
ambapo Mkurugenzi alionekana kuhusika na makosa kwa kuwakumbatia
watendaji hali ambayo imesababisha kutokuwa na imani naye
Habari kwa hisani ya Rashid Mkwinda
|
Post a Comment