Basi lateketea, 65 wanusurika

ABIRIA 65 waliokuwa wanasafiri kwa basi la Kampuni ya Moro Best, jana walinusurika kifo baada ya basi hilo kuteketea kwa moto katika eno la Sanga Sanga mkoani Morogoro.
Taarifa zilizotufikia wakati tukienda mitamboni zilisema kuwa, basi hilo lilikuwa likitoka jijini Dar es Salaam kuelekea Kilombero, na kwamba chanzo ni hitilafu ya umeme na hivyo kuwaka moto na kuteketea lote pamoja na baadhi ya mizigo ya abiria.
Hata hivyo, chanzo chetu cha habari kilisema kuwa hakuna abiria yeyote aliyefariki wala kuumia katika ajali hiyo iliyotokea majira ya jioni na hivyo, harakati za kuwatafutia abiria usafiri mwingine zilikuwa zikiendelea.
Kuhusu hali ya usalama ni kwamba Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na abiria hao waliimarisha ulinzi wa mizigo, na hivyo hakuna upotevu wowote uliojitokeza kwa mali ziliokolewa.

Post a Comment

Previous Post Next Post