Dawa zamchelewesa Sajuki kurudi

http://1.bp.blogspot.com/-YQaEYjeTTik/T6PEUQzjXFI/AAAAAAAAG0E/5Q9I0fvhmzY/s1600/sajuki.jpgBAADA ya kufanikiwa kufanyiwa upasuaji wa uvimbe uliokuwa ukimsumbua mwigizaji na muongozaji wa filamu nchini, Juma Kilowoko ’Sajuki’, imeelezwa kwamba dawa anazozitumia kwa sasa ndizo zinazomchelewesha kurejea nchini.
Rafiki wa karibu wa msanii huyo, Dennis Sweya ’Dino’, alisema dawa ambazo Sajuki anazitumia kwa sasa zina nguvu sana kiasi cha kwamba anatakiwa kuwa chini ya uangalizi maalum wa wauguzi.
Dino alisema kwamba kadiri siku zinavyopita ndivyo Sajuki anavyoendelea vizuri na akawaomba Watanzania kuendelea kumuombea ili arudi nyumbani salama.
“Tunashukuru ndugu yetu Sajuki ameshafanyiwa upasuaji na anaendelea vizuri sana kwa kweli hivi sasa hawezi kurudi kwa kuwa anatumia dawa ambazo ni lazima asimamiwe na wauguzi lakini hali yake inaimarika kila kukicha,” alisema Dino.
Alisema kuwa juzi mchana aliweza kuongea na Sajuki mwenyewe kwa simu na sauti yake ilikuwa yenye kuleta faraja ikiwa imeimarika sana kulinganisha na wakati alipoondoka.
Sajuki alikuwa katika hali ngumu ya kuumwa kutokana na uvimbe kwenye ini ambao ulimsababisha kupungua uzito na kutokana na kutokuwa na fedha za kugharamia matibabu nchini India ilibidi aombe msaada kutoka kwa wasamaria wema ambao walifanikisha.

Post a Comment

Previous Post Next Post