SIWEZI KUWA NA URAFIKI NA WACHEZAJI WA MADRID - BUSQUETS

Busquets: Siwezi kuwa na urafiki na wachezaji wa Madrid
Kiungo wa timu ya taifa ya Hispania na klabu ya Barcelona Sergio Busquets ametanabaisha kuwa hakuna hali ya kuelewana kati yake na wachezaji wa Real Madrid ndani ya kambi ya timu ya taifa ya Hispania. Ikumbukwe kuwa wiki hii kiungo wa klabu ya Barcelona  Xavi alitumia muda mwingi kuiponda Real Madrid pamoja na kocha wao Jose Mourinho. “Hapa kila mtu anafanya juhudi kubwa kwa ajili ya timu ya taifa, na kwa matatizo yoyote yanayojitokeza tunatakiwa tuyaache nje ya uwanja, Kila mchezaji anataka kuonekana bora. Ni ukweli usiofichika kuwa kuna kipindi inatokea mambo kutokwenda sawa kutokana na mikwaruzano ya hapa na pale, ila kwa sasa kila kitu kipo sawa kwani sisi wote lengo letu ni moja. Kiukweli ni ngumu sana kwa mchezaji kuwa na urafiki na mchezaji mwenzake ambaye hacchezi klabu moja na yeye hasa kwa zile timu pinzani.”

Post a Comment

Previous Post Next Post