Mapambano makali yatokea Damascus

Mji wa DamascusRipoti kutoka Damascus zinaonesha mapambano makali baina ya wanajeshi wa serikali na wapiganaji wa upinzani yametokea katika mji mkuu.
Walioshuhudia matukio hayo wanasema wapiganaji wa Jeshi Huru la Syria walifanya mashambulio yaliyopangwa dhidi ya vituo vya serikali siku ya Ijumaa.
Kinu cha umeme kilishambuliwa na moshi ulitanda.
Basi lilobeba wafanyakazi wa sekta ya mafuta kutoka Urusi lilipigwa.
Mashahidi wanasema wapiganaji wengi waliohusika waliuwawa au kukamatwa.
Haijulikani jeshi la serikali lilipata hasara gani na wakuu mjini Damascus hawakusema kitu juu ya tukio hilo.
Chanzo:- BBC Swahili

Post a Comment

Previous Post Next Post