MKATABA KATI YA TANZANIA NA UJERUMANI WASAINI MKATABA

MKATABA KATI YA TANZANIA NA UJERUMANI WASAINI MKATABA

NA MWANDISHI WETU
SERIKALI ya Tanzania na Ujerumani zimetia saini mkataba ambao utaruhusu wenzi na wategemezi wa ‘Diplomasia’ kufanya kazi kwenye nchi hizo.

Mkataba huo umesainiwa jijini Dar es Salaam jana,  na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa John Haule, akishirikiana na Balozi wa nchi hiyo Klaus Peter Brandes. 
Haule alisema kuwa, Tanzania ni ya pili kusaini mkataba kama huo, ya kwanza ilikuwa ni nchi ya Zambia.
Vile vile alifafanua kwamba ingawa Tanzania si mara yake ya kwanza kusaini mkataba na nchi nyingine lakini inaonesha ni jinsi gani inatambulika ndani na nje ya nchi hususan katika shughuli za maendeleo.
Aidha, aliitaja moja ya faida ya mkataba huo ni kuwasaidia watu hao kuendeleza taaluma zao sanjari na kupanua wigo wa kipato baina ya mtu  mmoja pamoja na familia.
“Kwa sasa Tanzania imeshaingia mkataba na nchi ya Canada, Marekani, pamoja na Ujerumani kuna haja ya kushirikiana, ukichukulia kwamba nchi yetu ni moja ya nchi yenye amani na inatambulika kwa sifa hiyo, hivyo muungano huu utatuwezesha kufanya kazi kwa uhuru bila kujali huko nchi za ugeni”alibainisha Haule.

Naye Balozi wa nchi hiyo Klaus Peter Brandes alisema mkataba huo umeonyesha ushirikiano mkubwa kati ya nchi hizo mbili, na utaendelea kuleta mafanikio makubwa kwa siku za mbele.

Post a Comment

Previous Post Next Post