TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAKABIZI
GARI MPYA AINA YA FORD FIGO KWA MSHINDI WAKE.
NI KATIKA PROMOSHENI YA VUMBUA HAZINA
CHINI YA KIZIBO NA SBL.
July 3, 2012,
Dar Es Salaam:
Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia vinywaji
vyake aina ya Serengeti Premium Lager, Tusker Lager na Pilsner Lager inaendesha
promosheni ijulikanayo kama vumbua hazina chini ya kizibo. Promosheni hiyo
inaendeshwa nchi nzima ambapo katika droo ya nne iliyochezeshwa katika ofisi za
kampuni hiyo zilizopo maeneo ya Oysterbay
jijini Dar Es Salaam alipatikana mshindi wa gari mpya aina FORD FIGO
aliyefahamika kwa jina la Isack Juvenary mwenye umri wa miaka 25 mkazi Morogoro.
Leo asubuhi katika ofisi za CMC zilizopo barabara ya azikiwe mkabala
na jengo la maktaba square jijini Dar Es Salaam, mamia ya watanzania kupitia vyombo vya habari
wameshuhudia kampuni hiyo ikimkabidhi zawadi hiyo ya gari mshindi wake bwana
Isack Juvenary jiji Dar es Salaam.
Akiongea na wandishi wa habari wakati wa kukabidhi zawadi hiyo, meneja
wa bia ya Serengeti Premium Lager Bw. Allan Chonjo amesema “Najisikia faraja
kubwa sana ninapoona yale tuliyoyapanga kuyatimiza kwa wateja wetu kama SBL na
kwamba hii ni sehemu tu ya yale yoye tuliyopanga kufanya kwa jamii
inayotuzunguka kwa kuthamini mchango wa wateje wetu na pia sisi tumelenga
katika kuwapa mabadiliko katika maisha yao kwa kuzingatia mahitaji muhimu ya
binadamu, na ndiyo maana tuna zawadi za magari, Bajaji, majenerata na pikipiki
ili ziwasaidie katika shughuli zao za kila siku na pia fedha taslimu kuanzia
shilingi elfu kumi, elfu hamsini na laki moja ambazo unaweza kushinda” alisema
Chonjo huku akisisitiza kuwa promosheni hiyo bado inaendelea kwa wiki takriban
saba zijazo na kuwataka watanzania wote wenye sifa zilizoainishwa katika vigezo
na masharti vya promosheni hiyo kushiriki kwa wingi ili kuongeza uwezo
wakushinda zawadi mojawapo.
MAELEKEZO:
Nunua bia ya serengeti lager, Tusker lager au Pilsner
Lager fungua kisha angalia chini ya kizibo utapata namba zilizopo katikati ya
kizibo, Fungua sehemu ya kutuma ujumbe mfupi kwenye simu yako, nakili namba
hizo mfano 55550, kisha tuma namba
zilizopo pembezoni mwa kizibo. Fanya hivyo kwa kufuata maelekezo katika
vipeperushi na magazeti. Pia unaweza
kujipatia bia ya bure papo hapo kila ubanduapo kizibo cha bia zote tatu
zilizoainishwa katika promosheni hii.
Haiuzwi kwa walio chini ya miaka kumi na minane.
Serengeti
Breweries Limited ni kampuni tanzu ya EABL/ DIAGEO.
Kwa
mawasiliano zaidi wasiliana na SBL Mkurugenzi wa mahusiano na mawasiliano, Mrs.
Teddy Mapunda at teddy.mapunda@diageo.com; Tel +255 784 747 665nakupitiaDrinkQ.com
MWISHO/
Post a Comment