CAMP NOU YAMNYAKUA SONG, SAHIN AJA EMIRATES KUZIBA PENGO LAKE.

CAMP NOU YAMNYAKUA SONG, SAHIN AJA EMIRATES KUZIBA PENGO LAKE.

On his way: Alex Song is expected to complete his proposed move to Barcelona imminently
Alex Song anaenda Barcelona
KIUNGO wa kimataifa wa Cameroon, Alex Song anatarajiwa kutua Barcelona leo kukamilisha uhamisho wa pauni Milioni 15 katika klabu hiyo ya Nou Camp - wakati huo huo, Arsenal inakwenda mbio kukamilisha usajili wa mkopo wa Nuri Sahin kutoka Real Madrid, awe mbadala wake. 
Arsenal inajiamini itampata Sahin wiki ijayo kutokana na kiungo wa Uturuki, ambaye pia ana pasipoti ya Ujerumani kuonyesha nia ya kujiunga na klabu hiyo ya London, kuliko Liverpool, ambao pia wanamtaka. 
Real Madrid pia kwao ni bora Sahin aende Anfield kwa sababu watapata ada kubwa ya mkopo, lakini watapingana na nia ya mchezaji kutaka kwenda Emirates. 
Arsenal pia inatumai, winga Theo Walcott atasaini mkataba mpya mwezi ujao, kutokana a mkataba wake wa sasa kuwa inausha mwishoni mwa msimu na mazungumzo yanaendelea.
Klabu hiyo inafikiri wachezaji wapya Lukas Podolski, Santi Cazorla na Olivier Giroud, watamshawishi kubaki, licha ya Robin van Persie kuondoka.  Arsenal inaweza kusajili kiungo mwingine mkabaji, kutoka Rennes, Yann M'Vila kwa dau la pauni Milioni 8. 
Kocha Arsene Wenger alisema: "Tutasajili kiungo mwingine. Lazima tuwe vizuri.'  Song, mwenye umri wa miaka 24, aliyejiunga na Arsenal akiwa ana umri wa miaka 18 kutoka Bastia , mwaka 2005, atakamilisha uhamisho wake leo na Barca inatumai kumtangaza rasmi kesho.
Akifafanua juu ya uamuzi wa kumuacha Song aondoke, Wenger alisema: 'Ameonyesha nia yake ya kwenda Barcelona. LakiniJack Wilshere anarudi ndani ya mwezi mmoja na nusu. Pia tuna Abou Diaby, ambaye amerejea baada ya kupona maumivu yake, na Tomas Rosicky hayuko mbali. 
'Inachanganya (wachezaji wanapoondoka) lakini tumejifunza kupambana na hali hiyo, na ushawishi wa kifedha wa klabu nyingine ni mkubwa. Mbalo linafanya tofauti.' 
Song anatakiwa na Barca akawe msaidizi wa Sergio Busquets na walipandisha dau lao baada ya mchezaji ambaye walimtaka awali kama chaguo lao la kwanza, Javi Martinez, anataka kwenda Bayern Munich kwa pauni Milioni 35

Recruitment drive: Arsenal are hoping to land Nuri Sahin from Real Madrid on loan

Nuri Sahin wa Real Madrid atatua Arsenal kwa mkopo
 

Post a Comment

Previous Post Next Post