MAGAZETI ULAYA NA TETESI ZA UAMISHO LEO HII(ROONEY,WALCOTTSTEWART NA WENGINE FUATILIA)

ROONEY AUZWA PAUNI MILIONI 40

Wayne Rooney anahofia Manchester United inajiandaa kumuuza kwa pauni Milioni 40. Na hofu hiyo inakuja baada ya kusajiliwa Robin van Persie kutoka Arsenal.
Habari kamili: Daily Mirror

Theo WalcottWinga wa England, Theo Walcott amekataa ofa ya kusaini mkataba mpya Arsenal na anaweza kuuzwa kwa pauni Milioni 15 na klabu za Manchester City na Liverpool zipo mstari wa mbele kumsaini nyota huyo mwenye umri wa miaka 23.
Habari kamili: The Times (subscription only)

Newcastle itakubali ofa za kuwauza beki Muargentina, Fabricio Coloccini, mwenye umri wa miaka 30, kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast, Cheick Tiote, mwenye umri wa miaka 26, au kiungo Mfaransa, Yohan Cabaye, mwenye miaka 26 pia.
Habari kamili: Independent

Wakala wa Dimitar Berbatov amekwenda Florence kufanya mpango wa uhamisho wa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Bulgarian kutoka Manchester United kwenda Fiorentina.
Habari kamili: Gazetta dello Sport (in Italian)

Stewart DowningKocha wa Liverpool, Brendan Rodgers amemuonya Stewart Downing kwamba winga huyo anaweza kurudishwa beki ya kushoto ili kupata nafasi ya kuendelea kuishi Anfield.
Habari kamili: Guardian

Kiungo wa Arsenal, Mikel Arteta ameelezea jinsi alivyochanganyikiwa na jinsi wachezaji wapya wanavyokabiliwa na changamoto ya kuchanganya haraka, baada ya kuondoka kwa nyota Robin van Persie.
Habari kamili: Metro

Post a Comment

Previous Post Next Post