OCHIENG KUPATA ITC YAKE LEO
![]() |
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe kushoto akimkabidhi jezi Paschal Ochieng baada ya kusaini mkataba na klabu hiyo. Katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange 'Kaburu' |
SIMBA SC imemaliza
utata wa usajili wa beki wake wa kimataifa wa Kenya, Paschal Ochieng kutoka AFC
Leopard ya Kenya na sasa hakuna shaka atachezea Wekundu hao wa Msimbazi msimu
mpya.
Habari za ndani kutoka
Simba SC, zimesema kwamba, Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, chini ya Mwenyekiti
wake, Zacharia Hans Poppe ilikutana na klabu hiyo bingwa ya zamani ya Kenya na
kumaliza tofauti zao.
Leopard ilikuwa inadai
Simba imemsajili Ochieng kinyume na utaratibu, kwani bado ana mkataba na klabu
yake hiyo wa miezi sita.
Kwa sababu hiyo, Hati
ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ya beki huyo wa zamani wa Yanga, inatarajiwa
kuwasili nchini kuanzia leo.
Ochieng
ni miongoni mwa wachezaji watano wa kigeni watakaokuwamo kwenye kikosi cha
Simba cha msimu ujao, wengine wakiwa ni kiungo Mussa Mudde, ambaye hata hivyo
inaelezwa anaweza kukatwa akasajiliwa Keita wa Mali, washambuliaji Felix Sunzu
kutoka Zambia, Emmanuel Okwi kutoka Uganda na Daniel Akuffo kutoka Ghana.
Post a Comment