MILIONI 80 KUONDOE PINGAMIZI LA YONDAN,WAO WAPAMBANA NA PINGAMIZI LA REDONDO - SIMBA

Redondo

Jitihada za chini zinaendelea kwa viongozi wa Simba SC, kuhakikisha wanamalizana na klabu ya Azam FC juu ya kiungo Ramadhani Chombo ‘Redondo’, aweze kuichezea klabu hiyo katika Ligi Kuu.

Azam inapinga usajili wa Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kwenda Simba kwa maelezo bado ina mkataba naye unaomalizika Juni 11 mwakani na ili kumuachia kiungo huyo iliyemsajili kutoka Simba miaka mitatu iliyopoita, inataka dola za Kimarekani 50,000 ingawa Simba wamefika dola 20,000 ambazo pia wameomba kulipa kwa awamu.
Habari zaidi zinasema kwamba, Simba nayo inataka dola 60,000, zaidi ya Sh. Milioni 80 kutoka kwa Yanga, ili wawauzie beki Kevin Yondan. Simba imepinga Yondan kusajiliwa Yanga kwa maelezo kuwa ina mkataba naye uliosainiwa Desemba 23 mwaka jana.
Vilevile Simba imewasilisha malalamiko ya mchezo usio wa kiungwana katika usajili wa Mbuyu Twite aliyeko Yanga kwa maelezo alisaini mkataba na klabu yao Agosti Mosi mwaka huu mbele yao, viongozi wa Shirikisho la Soka Rwanda (FERWAFA) na APR ambapo alilipwa dola 30,000 na nyingine 20,000 ikiwa ni fedha ya kujikimu na nauli yake ya kujiunga na klabu hiyo.
Nayo Yanga inapinga Simba kuwaacha wachezaji Dan Mrwanda, Haruna Shamte, Kanu Mbiyavanga na Lino Masombo kwa maelezo walishapatiwa leseni za kucheza Ligi ya Tanzania walizozitumia kwenye mashindano ya Kombe la Kagame. Pia inapinga Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kujiunga Simba kwa vile ana leseni ya kuchezea Azam kwa msimu wa 2012/2013.
Pingamizi lingine la Yanga kwa Simba ni kuwa imezidisha idadi ya wachezaji wa kigeni wanaotakiwa kusajiliwa kwa maelezo inao wanane wakati wanaoruhusiwa ni watano. Imewataja wachezaji hao kuwa ni Lino Masombo, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Mussa Mude, Kanu Mbiyavanga, Pascal Ochieng, Komalmbil Keita na Daniel Akuffor.
Pingamizi nyingine Zaidi bofya hapa

Post a Comment

Previous Post Next Post