Mtu
mmoja akatwa kichwa Zanzibar na hapa ndipo ulipopatikana mwili wa mtu
kisimani ukiwa hauna kichwa. kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa
mjini magharibi Aziz Juma Mohammed amesema mtu mmoja aliyetambuliwa kwa
jina la Seif Othman Mkumbo mwenye umri kati ya miaka 70 na 80 amekatwa
kichwa na mwili wake kutupwa katika kisima cha Kwa Raju Kikwajuni au
sijui niseme Maisara. Jeshi la Polisi limemkamata kijana aitwae Salum
Khamis Said akiwasaidia polisi kwa upelelezi zaidi juu ya tukio hilo.
Taarifa zaidi zinasema kwamba Mzee Seif hajaonekana kwa siku tatu
katika eneo lake la kazi wakati kumbe alikuwa tayari ameshakufa na awali
wa kujulikana mkasa huo ni watumiaji wa kisima hicho walisikia harufu
mbaya katika maji wanayotumia na ndio kijana Salum ambaye ni mlinzi wa
hapo sehemu ya baa ya kwa Raju alipowaita wasafishaji wa kisima na ndipo
walipochungulia na kuona mwili wa mtu na wakaitwa polisi kuja
kushuhudia na kutoa maiti hiyo ambayo ilikuwa tayari imeshaharibika hadi
sasa kichwa chake hakijapatikana lakini polisi wanamshikilia kijana
ambaye alikuwa akiishi na Mzee huyo
Taarifa zaidi zinasema kwamba Mzee Seif hajaonekana kwa siku tatu katika eneo lake la kazi wakati kumbe alikuwa tayari ameshakufa na awali wa kujulikana mkasa huo ni watumiaji wa kisima hicho walisikia harufu mbaya katika maji wanayotumia na ndio kijana Salum ambaye ni mlinzi wa hapo sehemu ya baa ya kwa Raju alipowaita wasafishaji wa kisima na ndipo walipochungulia na kuona mwili wa mtu na wakaitwa polisi kuja kushuhudia na kutoa maiti hiyo ambayo ilikuwa tayari imeshaharibika hadi sasa kichwa chake hakijapatikana lakini polisi wanamshikilia kijana ambaye alikuwa akiishi na Mzee huyo

Post a Comment