 |
| Mwadini
Ali akiruka bila mafanikio kuokoa mpira uliopigwa na Felix Sunzu na
kuipatia Simba bao la kusawazisha katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba ilishinda 3-1. |
 |
| Kocha wa Azam, Boris Bunjak na Msaidizi wake, Kali Ongala wakishuhudia kipigo |
 |
| Azam wakipiga ndiki kabla ya mechi |
 |
| Nahodha wa Simba, Juma Kaseja akisali kabla ya mechi |
Picha na Bin Zubeiry( http://bongostaz.blogspot.com/)
 |
| Kaseja akishukuru baada ya sala |
 |
| Salum Abubakr akipiga mpira |
 |
| John Bocco akielea kushangilia baada ya kufunga |
 |
| Bocco akichechemea baada ya kuumia |
 |
| Salum Abubakar katikati ya wachezaji wa Simba, Jonas Mkude kulia na Okwi kushoto |
 |
| Benchi la Azam |
 |
| Shomary Kapombe akimdhibiti Samir Hajji Nuhu |
 |
| Kaseja akiwapanga mabeki wake wakati wa kona |
 |
| Kipre Tcheche akimtoka Paschal Ochieng |
 |
| Samir Hajji Nuhu akitafuta mbinu za kumtoka Kapombe |
 |
| Kapombe baada ya kumpokonya mpira Nuhu anaondoka nao |
 |
| Okwi akitafuta mbinu za kumtoka Ibrahim Shikanda wa Azam |
 |
| Juma Kaseja akisujudu baada ya Simba kusawazisha bao |
 |
| Simba wakipongezana baada ya bao la pili |
 |
| Mkude akimiliki mpira |
 |
| Ochieng akizungumza na Kaseja |
 |
| Ngassa anasafiri |
 |
| Himi Mao Mkami akimtoka Mwinyi Kazimoto |
SIMBA SC imezinduka kutoka kwenye wimbi la sare katika Ligi Kuu
ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kufanikiwa kuichapa Azam FC mabao 3-1 kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Simba izidi kujitanua kileleni mwa
ligi hiyo kwa kufikisha pointi 22, baada ya kucheza mechi 10, wakati Azam FC
inabaki nafasi ya pili kwa pointi zake 18, baada ya kucheza mechi tisa.
Mabao ya Simba leo yalitiwa kimiani na Emanuel Arnold Okwi
mawili na Felix Mumba Sunzu Jr. moja, wakati la Azam lilifungwa na John Raphael
Bocco ‘Adebayor’.
Hadi mapumziko, tayari Simba walikuwa mbele kwa mabao 2-1,
Azam wakitangulia kufunga dakika ya nne, kupitia kwa Adebayor ambaye alimtoka
beki Mkenya Paschal Ochieng na kumchambua Juma Kaseja.
Dakika mbili baadaye, Sunzu aliisawazishia Simba, akiunganisha
kwa kichwa krosi maridadi ya Mrisho Khalfan Ngassa kutoka wingi ya kulia.
Okwi aliifungia Simba bao la pili dakika ya 40, baada ya
kutokea kizaazaa langoni mwa Azam kufuatia mpira uliopigwa langoni mwa timu
hiyo na Mwinyi Kazimoto.
Kipindi cha pili Simba walirudi na moto wao na iliwachukua
dakika tano tu kuhitimisha karamu yao ya mabao, baada ya Okwi kuwainua tena
vitini mashabiki wa Simba, akifumua shuti la umbali wa mita 19, baada ya kuwatoka
mabeki wa Azam.
Mrisho Ngassa ndiye alikuwa nyota wa mchezo wa leo, kutokana
na kuisumbua mno Azam, iliyomuuza kwa mkopo Simba miezi miwili iliyopita.
Simba SC; Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Amir Maftah, Paschal
Ochieng, Shomary Kapombe, Jonas Mkude, Amri Kiemba/Ramadhan Chombo, Mwinyi
Kazimoto, Felix Sunzu/Ramadhan Singano, Mrisho Ngassa/Christopher Edward na Emmanuel
Okwi.
Azam FC; Mwadini Ali, Ibrahim Shikanda, Samir Hajji Nuhu,
Said Mourad na Aggrey Morris, Abdulhalim Humud, Jabir Aziz/Abdi Kassim, Himid
Mao/Kipre Balou, John Bocco ‘Adebayor’/Khamis Mcha, Kipre Herman na Salum
Abubakar.
Katika mchezo uliotangulia, Azam B iliifunga Simba B 1-0, bao
pekee la Kevin Friday dakika ya 56.
Kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha, Yanga iliibuka
na ushindi wa 1-0, bao pekee la beki Mbuyu Twite, hilo likiwa bao lake la tatu
tangu ajiunge na timu hiyo kwenye ligi hiyo.
Kwa ushindi huo, Yanga imetimiza pointi 17, baada ya kucheza
mechi 10 na inaendelea kusimama katia nafasi ya tatu.
Mechi nyingine za ligi hiyo leo ni kati ya African Lyon na
Kagera Sugar Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam, Mgambo JKT na Prisons Uwanja wa Mkwakwani,
Tanga na Ruvu Shooting dhidi ya Polisi Morogoro Uwanja wa Mabatini, Mlandizi.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo miwili kati ya JKT
Ruvu na Coastal Union Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam na Toto Africans dhidi
ya Mtibwa Sugar Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
 |
| Ochieng amelala kuondosha mpira miguuni mwa Kipre Tcheche, huku Amri Kiemba akiwa tayari kumsaidia |
 |
| Mkude anaondoka na mpira mbele ya Abubakr wa Azam, huku Amir Maftah akiwa tayari kumpa msaada |
 |
| Bocco anamtoka Ochieng |
 |
| Simba wakishuangilia bao la Sunzu |
 |
| Rafu iliyomtoa nje Bocco, aligongana na Kiemba |
 |
| 11 wa Simba walioipiga Azam leo |
 |
| Humud akiwa hewani na Sunzu |
 |
| Ngassa anawatoka wachezaji wa Azam |
 |
| Ngassa anamuwajibisha Said Mourad |
 |
| Okwi akijiandaa kufunga bao la tatu |
 |
| Mwadini pamoja na kufunhgwa matatu, lakini aliokoa ya kutosha |
 |
| Ulinzi ulikuwa mkali, lakini Okwi alipiga mbili |
 |
| Kiungo wa zamani wa Azam na Simba, Shekhan Rashid akishuhudia mechi hiyo. Kushoto ni mmoja wa viongozi wa Azam, Heri Mzozo |
Post a Comment