HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA UWANJA WA MKWAKWANI MJINI TANGA,SIMBA ALIPOSHIKWA KOO NA COASTAL

Wa pili kutoka kulia mdhamini mkuu wa Coastal Union, Nassor Bin Slum akiwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani leo wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Simba, ambayo iliisha kwa sare ya bila kufungana. 

Mwenyekiti wa Friends O Simba, Zacharia Hans Poppe aliyeinua mkono 

Kutoka kulia Hans Poppe, Evans Aveva na Pamba

Hans Poppe

Ben Mwalala kulia

Kocha Mkuu wa Costal, Ahmad Morocco kulia akijadiliana na Kocha wa makipa wa timu hiyo, Juma Pondamali

Makchaa wa Vituko Show

Mashabiki wa Simba

Waandishi wa Habari

Waandishi wa habari. Katikati ni Mhariri Mtendaji wa Mwanaspoti, Frank Sanga

Nahodha wa Simba Juma Kaseja akiwaongoza wachezaji wake kuingia uwanjani

Haruna Moshi 'Boban' akifurahi na Juma Jabu wakati timu zinaingia

11 wa Simba walioanza leo

11 wa Coastal walioanza leo

Felix Sunzu anasafiri

Sunzu anashughulika

Kiungo chipukizi wa Simba, Haroun Chanongo akipasua msitu wa mabeki wa Coastal

Nassor Masoud 'Chollo' katika msitu wa wachezaji wa Coastal akipasua

Chollo huyo

Chollo huyoo

Jerry Santo wa Coastal akijaribu kumdhibiti Chollo

Mwisho wa safari ya Chollo

Sunzu akidhibitiwa

Chollo katika mishe

Haroun Chanongo anateleza

Haroun huyo

Haroun anamtoka Saidi Swedi Nahodha wa Coastal

Haroun anamuacha Swedi

Haroun anatia krosi

Hatari kwenye lango la Simba

Juma Kaseja anadaka

Hatari kwenye lango la Simba

Paschal Ochieng anaokoa

Jerry Santo katika msitu wa wachezaji wa Simba

Suleima Kassim 'Selembe' wa Coastal akipagombea mpira na Haruna Moshi 'Boban' wa Simba

Kipa wa Coastal, Jackson Chove akidaka mpira mbele ya Daniel Akuffo wa Simba. Kulia ni Nahodha Saidi Swedi akiwa tayari kutoa msaada  

Chove akiwadaka huku akiugulia maumivu ya kuumizwa na Akuffo

Chove amedaka, Sunzu chini

Sunzu anamiliki mpira mbele ya Razack Khalfan

Razack Khalfan anasafiri, Sunzu ameangukia goti 

Wachezaji wa Simba na Coastal wakigombea mpira

Cheki kazi hiyo

Mapumziko, kila kila ikisema na Mungu wake...kulia Coastal, kushoto Simba SC

Kiungo wa zamani wa Coastal, Titus Bandawe kulia akizungumza na Saad kawemba wa TFF 

Razack Khalfan anatolewa nje, hakurudi..

Shughuli

Atupele Green wa Coastal akichanja mbuga

Atuepele anajaribu

Amri Kiemba anamtoka Saidi Swedi kulia

Sunzu leo alishughulika sana

Kaseja anasema na mabeki wake

Santo anatoa pasi

Kiemba anapasua

Hatari kwenye lango la Simba

Amir Maftah anasafiri

Saidi Swedi cbini, baad aya kukumbana na Maftah


Sunzu akidhibitiwa

Sunzu aliupitia mira mikononi mwa Chove

Chove anampiga mkwara Sunzu baada ya kuupitia mpira mikononi mwake 


Shughuli

Uhuru Suleiman kulia

Uhuru kulia

Kazi kazi

Hatari kwenye lango la Simba

Kaseja anawapanga mabeki wake

Haruna Moshi 'Boban' anamiliki mpira

Selembe chini

M ilovan hana hamu na Coastal

Wenye Simba yao 'wakisikia baridi'

Hapa Kaseja aliokoa bao moja la wazi sana

Boban na Swedi wakipongezana baada ya mechi

AZAM FC imepiga hatua kubwa kuelekea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom kufuatia ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Polisi mkoani Morogoro huku Simba ikidondosha pointi mbili katika sare ya 0-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga katika mechi ambayo wenyeji walimaliza wakiwa 10.

Goli pekee kutoka kwa straika raia wa Ivory Coast, Kipre Tchetche liliifanya Azam ifikishe pointi 16, moja nyuma ya mabingwa Simba wenye pointi 17 huku Wekundu wa Msimbazi wakiwa wamecheza mechi moja zaidi ya Azam.

Kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Coastal Union walilazimika kucheza dakika 25 za mwisho wakiwa 10 baada ya straika wao nyota Nsa Job kutolewa kwa kadi ya pili ya njano katika dakika ya 65. 


Katika mechi nyingine za leo, kwenye Uwanja wa Manungu, wenyeji Mtibwa Sugar walichapwa 2-1 na timu ya Mgambo JKT ya Tanga, ikiwa ni ushindi wake wa pili mfululizo baada ya kuanza na vipigo vinne mfululizo tangu ilipopanda daraja msimu huu.


Ruvu Shooting ilishinda 1-0 dhidi ya African Lyon kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi na Prisons ililala nyumbani 1-0 dhidi ya JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.


 Vikosi katika mechi ya Tanga vilikuwa:

Coastal:
Jackson Chove, Said Swedi, Juma Jabu, Mbwana Hamisi, Jamal Machelanga/Ismail Khamis, Jerry Santo, Mohamed Athumani/Daniel Lyanga, Selemani K Selemani, Atupele Green, Nsa Job na Razack Khalfan/Lameck Mbonde.  

Simba:
Juma Kaseja, Nassor Said 'Cholo', Pascal Ochieng, Shomary Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Haruna Moshi ‘Boban’, Felix Sunzu, Daniel Akuffor/Salim Kinje na Haroun Chanongo/Uhuru Suleiman.
Picha na:- Bin Zubeiry 
Milovan baada ya filimbi ya mwisho

Post a Comment

Previous Post Next Post