![DSCN6190](http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2012/10/DSCN6190.jpg)
Picha
mbali mbali za tukio la kupigwa kwa bomu nyumbani kwa katibu wa bakwata
mkoa wa Arusha Abdul Kareem Jonjo (Pichani akiwa Hospitalini) na baadhi
ya vongozi wa ulinzi na usalama mkoa wa Arusha wakionngozwa na mkuu wa
mkoa wa Arusha wakiwa kwenye matukio mbali mbali nyumbani na hospitalini
jijini Arusha leo baada ya tukio la kupigwa kwa bomu kwa katibu huyo
nyumbani kwake eneo la mtaa wa kanisani kata ya Sokon 1 jijini
Arusha.(picha na zote na Mahmoud Ahmad).
![DSCN6193](http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2012/10/DSCN6193.jpg)
Mahmoud Ahmad Arusha
Kaimu
kamanda wa jeshi la polisi Zuberi Mwombeji ameelezea tukio la
kushambuliwa kwa bomu kwa katibu wa Bakwata mkoa wa Arusha na kusema
kuwa MNAMO TAREHE 25 mwezi huu MUDA WA SAA 6:30 USIKU KATIKA MTAA WA
KANISANI KATA YA SOKONI ONE ILIYOPO HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA, MTU
MMOJA ALIYEJULIKANA KWA JINA LA ABDULKARIMU IDD JONJO (52) KATIBU WA
BAKWATA MKOA WA ARUSHA NA NI MKAZI WA SOKONI ONE ALIJERUHIWA KWA MLIPUKO
KATIKA VIDOLE VYAKE VITATU VYA MKONO WA KULIA PAMOJA NA KIDEVUNI
TUKIO
HILO LILITOKEA CHUMBANI KWAKE KATIKA NYUMBA ALIYOPANGA AMBAYO
INAMILIKIWA NA JAPHET S URIO. TAARIFA ZA AWALI ZINAELEZA KWAMBA, NDUGU
ABDULKARIMU IDD AKIWA USINGIZINI GHAFLA ALISHTUSHWA NA SAUTI YA
KISHINDO KILICHOTOKEA DIRISHANI NA MARA BAADA YA KUAMKA ALIONA KITU
KIKINING’INIA DIRISHANI NA ALIPOKIGUSA GHAFLA ULITOKEA MLIPUKO AMBAO
ULIMJERUHI KATIKA MAENEO YA MWILI WAKE YALIYOTAJWA HAPO JUU.
KUFUATIA
TUKIO HILO, ALIOMBA MSAADA KWA MAJIRANI AMBAO WALIMPELEKA HOSPITALI YA
MOUNT MERU KWA AJILI YA MATIBABU AMBAPO MPAKA HIVI SASA AMELAZWA KATIKA
HOSPITALI HIYO NA ANAENDELEA VIZURI.
Kaimu
kamanda alisema kuwa MARA BAADA YA JESHI LA POLISI KUPATA TAARIFA HIYO
BAADHI YA ASKARI WALIKWENDA KATIKA ENEO LA TUKIO NA KATIKA UCHUNGUZI WA
AWALI WALIBAINI KWAMBA MLIPUKO HUO ULIANZIA NDANI YA CHUMBANI HICHO NA
KUTOKEA NJE USAWA WA SAKAFU NA UKUTA, PIA KUMETOKEA UHARIBIFU WA VIOO
VYA DIRISHA MOJA NA VIPANDE VYAKE KUANGUKIA NJE NA PIA MADUMU MAWILI YA
LITA 10 YALIYOKUWA NA MAJI YALIPASUKA KWENYE VITAKO VYAKE NA MAJI HAYO
KUTAPAKAA KATIKA CHUMBA HICHO.
Kwa
mujibu wa kaimu kamanda wa jeshi hilo alisema kuwa MPAKA HIVI SASA
HAKUNA MTU YEYOTE ALIYEKAMATWA KUHUSIANA NA TUKIO HILO NA JESHI LA
POLISI MKOANI HUMO LINAENDELEA NA UPELELEZI WA KINA ILI KUWEZA KUBAINI
CHANZO, SABABU ZA KUTOKEA KWA TUKIO HILO NA HATIMAYE KUWAKAMATA WALE
WOTE WALIOHUSIKA NA TUKIO HILO.
Post a Comment