


Mshindi huyo wa tuzo za Grammy ameandika kwa ufupi na moja
kwa moja kwenye point iliyokuwa inasubiriwa na fans wake kuhusu afya yake,
japokuwa hakusema kilichomsibu hasa.
Alitweet “Thanx for all the prayers! I am good…” ilisomeka
hivi tweet ya october 27 ya mkali huyo wa michano.

Hivi karibuni Lil Wayne alilazwa hospitalini mara mbili
baada ya kupatwa na kile kinachosemekana kuwa ni “seizure” na mara ya mwisho
alizima akiwa katika private jet na kulazimika kuahirisha safari ambapo ndege
hiyo ilitua na Weezy kukimbizwa hospitalini kwa matibabu, na wengi kuunganisha
ugonjwa huu na matumizi ya madawa ya kulevya.
Lakini management ya Weezy ilitoa taarifa ambazo hazikujibu
hasa rumors hizo zilizokuwa zinatapakaa kwenye mitandao mbalimbali, na ikasema
alikuwa amepungukiwa maji na pia maumivu ya kichwa cha upande mmoja lakini
haikutoa sababu hasa ya hali hii.
Post a Comment