UZINDUZI WA FILAMU YA CID WAFANA

Tino akizungumza na na wageni waalikwa (hawapo pichani) muda mchache kabla ya uzinduzi rasmi.
Tino akiitambulisha timu ya kampuni yake kwa wageni waalikwa (hawapo pichani).
Tino (katikati) akionesha cheti cha ubalozi wa watoto yatima mkoani Mbeya alichokabidhiwa ukumbini humo.
Mwakilishi kutoka kampuni ya magari ya Subaru (kulia) akimkabidhi Tino funguo za magari mawili ambayo kampuni hiyo imempatia kwa ajili ya kufanyia kazi zake za filamu za action.
Raisi wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba akizungumza jambo na wageni waalikwa (hawapo pichani).
Mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Maendeleo na Utamaduni nchini, Heman Mwansoko akizungumza na wageni waalikwa (hawapo pichani). Kushoto ni katibu wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Wilson Makubi, kulia ni raisi wa shirikisho hilo, Simon Mwakifwamba.
Mwigizaji Steve Mangere ‘Steve Nyerere’ (katikati) akiwa na wadau.
Wadau wakifuatilia uzinduzi.
Raisi Mwakifwamba (katikati) akiwa na baadhi ya waigizaji wa Bongo Movies.
USIKU wa kuamkia leo, mwigizaji mahiri Bongo, Hisani Muya ‘Tino’ alizindua filamu yake ya ‘action’ iitwayo C.I.D katika Ukumbi wa Business Park Makumbusho ambapo mastaa kibao wa fani mbalimbali walihudhuria kuinogesha.
PICHA/HABARI: ERICK EVARIST/GPL.

Post a Comment

Previous Post Next Post