Mkuu wa kitengo cha bidhaa wa Benki ya Baclays, Samuel
Mkuyu(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu
mshindi wa kwanza wa droo ya promosheni ya ‘Mkopo Bonanza’ ambaye atasamehewa
marejesho ya mkopo wake ya miezi kumi na mbili.Droo hiyo iliyochezwa Dar es
Salaam jana.Kulia ni Meneja wa Bidhaa wa benki hiyo, Adam Mbaga na Mkaguzi wa
Bodi ya michezo ya kubahatisha ya Taifa, Majid Bakari.
Meneja wa bidhaa wa Benki wa Baclays, Adam Mbaga
akichagua karatasi ya mshindi wa kwanza
ya droo ya promosheni ya ‘Mkopo Bonanza’ iliyochezeshwa Dar es Salaam
jana.Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya michezo ya kubahatisha Taifa, Majid Bakari na Mkuu wa kitengo cha bidhaa wa Benki ya
Baclays, Samuel Mkuyu
Mkuu wa kitengo cha bidhaa wa Benki ya Baclays, Samuel
Mkuyu(wa pili kushoto) akisoma jina la mshindi wa kwanza wa droo ya promosheni
ya ‘Mkopo Bonanza’ iliyochezwa Dar es Salaam jana.Kulia ni Kulia ni Mkaguzi wa
Bodi ya michezo ya kubahatisha Taifa, Majid Bakari na ni Meneja wa Bidhaa wa
benki hiyo, Adam Mbaga
Na Mwandishi Wetu.
BENKI ya
Barclays leo hii imehitimisha promosheni yake iliyojulikana kama “Barclays Mkopo Bonanza” kwa kuwapata washindi
wa bahati nasibu iliyochezeswa jijini Dar Es Salaam. Bahati nasibu hiyo
ilichezeshwa mbele ya waaandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari
na ilihudhuriwa pia na mwakilishi kutoka Bodi ya Taifa ya michezo ya
kubahatisha,Majidi Bakari
Akizungumza
na waandishi wa habari Bi. Sarah Munema, Meneja Masoko wa benki ya Barclays
alisema kwamba benki ya Barclays ilianza rasmi promosheni ya “Barclays Mkopo Bonanza” kuanzia mapema
mwezi wa tano mwaka huu. Kampeni hii ililenga kutoa mikopo kwa watu binafsi
ambao ni wafanyakazi wa serikali, makampuni na taasisi. Promosheni hii ilitoa
kivutio cha kutoa zawadi ya kusamehewa marejesho kwa kipindi fulani kwa wateja
wenye bahati watakaochaguliwa baada ya Draw kuchezeshwa mwishoni mwa promosheni
hii. Bi Sarah aliendelea kusema, “Promosheni hii ilikuwa na lengo la kuwapatia
wateja wa benki yetu nafasi ya kufikia ndoto zao kwa kuwapatia mikopo
itakayowapa uwezo wa kifedha wa kufanya yale wanayokusudia. Maelfu ya wateja
wetu wamenufaika na “Barclays Mkopo
Bonanza” na kama tulivyoahidi, leo
hii tuko hapa kwa ajili ya kuchezesha Draw itakayopata washindi watakaosamehewa
marejesho ya mikopo yao kwa vipindi maalum”. Alielezea kwamba mshindi wa kwanza
atasamehewa marejesho ya mkopo aliopata kwa kipindi cha miezi 12, hii itategemea
kiasi cha mkopo aliopata na marejesho aliyopangiwa. Washindi wengine ishirini
watajipatia zawadi ya kusamehewa kiasi cha marejesho yao ya mwezi mmoja kila
mmoja.
Naye
bwana Adam Mbaga, Meneja Bidhaa wa benki ya Barclays alielezea kwamba japokuwa
promosheni ya “Barclays Mkopo Bonanza” imemalizika
na washindi wa Draw kupatikana, benki bado inaendeleza huduma ya kutoa mikopo
kwa wafanyakazi wa serikali, makampuni na taasisi. Aliwahamasisha watu
mbalimbali kujitokeza kufungua akaunti na kufaidika na mikopo hii. Mikopo hii
inatolewa kwa wafanyakazi katika viwango tofauti hadi kufikia shilingi milioni
hamsini kwa mtu mmoja kutegemeana na kiasi cha mshahara wake.
Bi Sarah
Munema alimalizia kwa kutoa shukrani za dhati kwa wateja wote wa Barclays Bank
kwa kuchagua benki hii. Aliwaomba kujitokeza kwa wingi kutembelea matawi ya
benki hii kote Tanzania kufungua account na pia kuomba mikopo kwa ajili ya
kujiendeleza katika maisha yao ya kila siku.
Baada ya
kuchezeshwa draw ya bahati nasibu, washindi waliobahatika kupata zawadi ya
kusamehewa marejesho katika “Barclays
Mkopo Bonanza”
walikuwa ni;Washindi
ishirini
waliosamehewa marejesho ya mwezi mmoja ni;Carol Joseph,Jane
Hemed,Shaban Bakari,Paulina Gabriel,Abdalah Said,Idd Seleman,Mohamed
Athuman,Godliver Wiliam,Godfrey Beba,Zuberi Nungu,Ashura
Benedict,Richard Membu,Kulwa Gerge,Moses Joseph,Dastan Jemes,Jane
George,Peter Joseph,Obrien Zadose,Hadija Mohamed,Sangalali Michael.
Mshindi
wa kwanza aliyesamehewa marejesho ya miezi kumi na mbili ni;Veronza William ambaye ndeye mshindi wa kwanza
Post a Comment