CRDB YADHAMINI SHINDANO LA KUANDIKA MICHANGANUO YA BIASHARA KWA WANAFUNZI VYUO VIKUU.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezaeshaji Kiuchumi, Anaclet Kashuliza akizungumza wakati wa kuzindua shindano la kuandika michanganuo ya biashara litakalo shirikisha wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam lililodhaminiwa na Benki ya CRDB.

Amesema Ujasiriamali ni moja ya jitihada zinazoweza kumletea mtu binafsi,shirika na hata katika ngazi ya kijamii mabadiliko ya kimaendeleo iwapo fursa za kibiashara zinazopatikana zitatumika ipasavyo.
Bw. Kashuliza amesema ili fursa hizo ziweze kutumika kuleta maendeleo Wajasiriamali wanapaswa kupata elimu ya Ujasiriamali na kuifanyia kazi kwa vitendo na sio kuishia madarasani.
Ofisa Masoko wa CRDB, Emmanuel Kiondo akizungumzia malengo ya CRDB kudhamini  Shindano la kuandika mchanganuo wa biashara kwa wanafunzi wa Vyuo vikuu katika hafla ya uzinduzi wa shindano la kuandika michanganuo ya biashara na kuvishirikisha vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam. 
Country Managing Partner wa Ernest & Young Bw. Joseph Sheffu Country akizungumza machache wakati wa uzinduzi wa shindano la kuandika michanganuo ya biashara kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vya jijini Dar es Salaam ambapo amesema angependa kuona kadri siku zinavyokwenda tasnia ya Ujasiriamali inazidi kupanuka ikiwa na wataalamu wa kutosha.
Mkurugenzi wa Kitivo cha Ujasiriamali cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDEC), Maria Nchimbi akitoa nasaha kwa wanafunzi na kuwapongeza shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDBS) kwa kuandaa wazo hilo ambalo limepokelewa vyema na wadau wa biashara na hivyo kufikia kuandaliwa kwa mashindano hayo. 
 Afisa Mahusiano na Mawasiliano wa University Entrepreneurship Challenge 2012 Bw. Dennis Paul akitambulisha Kamati uliyofanikisha uzinduzi wa mashindano hayo na kutoa wito kwa makampuni na wadau wengine wajitoe kudhamini mashindano hayo.
Kamati ya maandalizi ya UNIVERSITY ENTREPRENEURSHIP CHALLENGE kutoka shule ya Biashara ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
 Pichani Juu na Chini ni  baadhi ya Wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali vya biashara vya jijini Dar es Salaam.

Mwanafunzi wa Mwaka wa tatu BCOM Accounting wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Joyce Wilfred Fungo akielezea marajio yake kujijenga kibiashara pindi atakapohitimu masomo.
Mgeni rasmi katika picha ya pamoja na uongozi wa UDEC.

Post a Comment

Previous Post Next Post