
Chidzambwa alifungiwa maisha na Chama cha soka cha Zimbabwe kwa kuhusika kwake na kupanga matokeo ya timu yao ya taifa kupoteza mechi kwa kudhamiria huko barani Asia katika kipindi cha kati 2007 na 2009 kwa malipo ya pesa kutoka kwa wacheza kamari wa huko Asia.
Kocha huyo wa zamani alituhumiwa kuwa ndio aliyepanga mchongo mzima kwa pamoja na Method Mwanjali wa Mamelodi Sundowns na mlinzi BidVest Wits Thomas Sweswe, ambao nao wamefungiwa maisha.
Lakini swali la kujiuliza ikiwa Chidzambwa tayari anatumikia adhabu ya kufungiwa maisha na FIFA, je shirikisho hilo la soka ulimwenguni ambalo mamlaka yake yanaishai kwenye soka tu, litampa adhabu gani nyingine kubwa kuzidi hiyo?
chanzo: shafih dauda
Post a Comment