Walivyoshiriki kuutafuna Mradi wa Mpunga
Kapunga
"TUNAWEZA kujibagua kutoka kwa
wenzetu kutokana na elimu tuliyonayo; tunaweza kujaribu kujilimbikizia wenyewe mali
haramu ya umma. Lakini gharama kwetu, pamoja na kwa ndugu zetu, itakuwa kubwa
mno. Itakuwa kubwa siyo tu kwa kushindwa kutimiza haja zetu, lakini pia kwa
usalama wetu na ustawi wetu." Haya ni maneno ya Mwalimu Julius Nyerere yaliyomo
katika kitabu chake cha Uhuru na Maendeleo cha mwaka 1973.
Nimeona
bora nianze na maneno haya ya Mwalimu Nyerere katika kuelezea kilichotokea
katika Mradi wa Umwagiliaji wa Mpunga Kapunga, ambao kwa hakika kama
ungeendelezwa vyema, ungekuwa mkombozi mkubwa kwa taifa katika suala zima la
chakula.
Muundo
wa uongozi katika mradi huo ulikumbwa na mabadiliko kadhaa wakati wa
uanzishwaji wake, ambapo kulionekana kuwa na “taasisi” mbili – Idara ya
Operesheni na Ukarabati na Kamati ya Menejimenti, nyongeza ambayo hata
wafadhili wenyewe wa mradi huo hawakuwahi kuiwaza kabla ya kuidhinisha mkopo.
Idara
ya Operesheni na Matengenezo iliongezwa Julai 1990 kwa lengo la kushughulikia
ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji, majengo na kazi nyingine za ujenzi.
Kuwepo kwake kulisaidia ukarabati wote katika kipindi hicho.
Endelea nayo....www.kwanzajamii.com/?p=4254

Post a Comment