 |
| Kipa
wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, ya Kongo
Brazzaville, Ombandza Mpea Joe akilalama baada ya mpira wa adhabu
uliopigwa na Mufathir Yahya Abbas kutinga nyavuni na kuwapa wenyeji
ushindi wa 1-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni ya leo. |
 |
| Bao pekee leo |
 |
| Kipa wa Kongo akining'inia kwenye milingoti ya lango baada ya kuukosa mpira uliopaa juu ya lango lake |
 |
| Mchezaji wa Serengeti, Suleiman Hamisi Bofu akipiga mpira kichwa mbele ya beki wa Kongo, Ondongo Boungena |
 |
| Beki Okombi Francis wa Kongo akiokoa mbele ya Joseph Kimwaga |
 |
| Wachezaji wa Kongo wakimdhibiti mchezaji wa Serengeti |
 |
| Hussein Twaha 'Messi' akiwafunga tela wachezaji wa Kongo |
 |
| Makocha
wa Serengeti Jacob Michelsen na Msaidizi wake Jamhuri Kihwelo wakiwapa
maelekezo vijana wao wakati mpira uliposimama kwa muda |
 |
| Kipa wa Serengeti Boys, Peter Manyika akiruka hewani kupangua mchomo mkali ulioelekezwa langoni mwake |
 |
| Kipa
wa Kongo, akimdondokea kiungo wa Serengeti, Farid Mussa Shah kudaka
mpira, huku beki wake, Ondongo Boungena akiwa tayari kumsaidia |
 |
| Farid kulia na Ondongo kushoto |
 |
| Kikosi cha vijeba wa Kongo Brazzaville |
 |
| Beki Ismail Adam Gambo wa Serengeti akimdhibiti Ibara Vinny wa Kongo Brazzazille |
 |
| Hussein Twaha akiwatoka wachezaji wa Kongo |
 |
| Serengeti wakishangilia bao lao kwa staili ya aina yake |
 |
| 11 wa kwanza wa Serengeti leo |
 |
| Wachezaji wa Serengeti Boys wakiimba wimbo wa taifa |
 |
| Benchi la Ufundi la Serengeti Boys wakati wa wimbo wa taifa |
 |
| Hussein Twaha akipasua katikati ya msitu wa wachezaji wa Kongo |
 |
| Hussein Twaha akimiliki mpira mbele ya beki wa Kongo |
 |
| Joseph Kimwaga akimtoka beki wa Kongo Brazzaville |
 |
| Beki wa Kongo Okombi Francis baada ya kumpitia kwanja Tumaini Baraka Mosha wa Serengeti |
 |
| Mudathir akiondoka na mpira |
 |
| Tumaini Baraka Mosha akimtoka Okombi |
 |
| Kushoto refa anasema twende, huku Tumaini Baraka Mosha akiwania mpira dhidi ya Ondongo |
TIMU ya
taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys leo imeifunga 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu na ya mwisho kuwania tiketi ya
kucheza Fainali za vijana wa umri huo Afrika zitakazopigwa nchini Morocco
mwakani.
Kwa matokeo
hayo, Serengeti sasa inahitaji hata sare yoyote katika mchezo wa marudiano wiki
mbili zijazo mjini Brazzaville ili kukata tiketi ya Morocco mwakani.
Kwa ujumla
Serengeti walipigana katika mchezo wa leo, kwani wapinzani wao walionekana kuwa
bora na wenye uzoefu zaidi yao.
Katika
mchezo huo uliochezeshwa na refa Miiro Nsubuga, aliyesaidiwa na Mark Ssongo,
Balikowa Ngobi na Ronnie Kalemba wote kutoka Uganda, hadi mapumziko Serengeti
walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililopatikana dakika ya 15.
Bao hilo
lilifungwa kwa shuti la mpira wa adhabu na beki Mudathir Yahya Abbas kutoka
umbali wa mita 22 na mpira kabla ya kutinga nyavuni ulimbabatiza beki mmoja wa
Kongo na kumpoteza njia kipa Ombandza Mpea Joe na kujaa nyavuni.
Faulo hiyo
ilitokana na kiungo wa Serengeti, Hussein Twaha Ibrahim ‘Messi’kuangushwa na
beki Okombi Francis wakati akiwa analekea kwenye eneo la hatari la Wakongo.
Baada ya bao
hilo, Wakongo walijaribu kuongeza jitihada kiuchezaji, lakini ukuta imara wa
Serengeti ulioongozwa na kipa Peter Manyika uliwazuia kusawazisha hadi dakika
45 za kipindi cha kwanza zinatimia.
Baada ya
mechi hiyo, kocha wa Serengeti Boys, Mdenmark, Jacob Michelsen aliwapongeza
vijana wake, lakini akasema bado wana kazi kubwa mbele yao.
Kocha wa
Kongo, Mfaransa Eddie Hudanski alitolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 88, baada
ya awali kuonywa kwa kutoa lugha chafu, lakini akarudia.
Refa Nsubuga
alitoa kadi moja tu ya njano kwa Issambey Lonvreve aliyeingia kipindi cha pili
kuchukua nafasi ya Ibara Vinny.
Tanzania; Peter Manyika Peter, Miza Kriston
Abdallah, Mohamed Hussein Mohamed, Ismail Adam Gambo, Miraj Adam Suleiman,
Mudathir Yahya Abbas, Mohamed Salum Haroub, Joseph Kimwaga Lubasha/Dickson
Isaac Ambundo, Hussein Twaha Ibrahim, Suleiman Hamisi Bofu/Tumaini Baraka Mosha
na Farid Mussa Shah.
Kongo Brazzaville; Ombandza Mpea Joe, Tmouele Ngampio,
Mabiala Gharlevy, Okimbi Francis, Ondongo Boungena, Ibra Vinny/Issambey Lonvreve,
Binguila Handy, Obassi Ngatsongo, Mohendiki Brel, Atoni Mavoungou na Biassadila
Arei.
Picha na Bin Zubeiry
Post a Comment