Kunradhi,kuna
tatizo la kiufundi kwenye kamera ya msaidizi wa mwenyekiti,ndiyo maana
makala haiwezi kusomeka vizuri kwenye gazeti.isome hapa chini
Cazorla wa Arsenal angefungiwa mechi
tatu
Na Olle Bergdahl Mjengwa,
KATIKA
mchezo wa mpira kuna wachezaji wengi wanaopenda kujiangusha bila kuguswa. Wachezaji
hawa wanaharibu mchezo wa mpira. Nitawapa mfano uliotokea wiki mbili zilizopita.
Arsenal walicheza mechi dhidi ya Westbrom. Katika kipindi cha kwanza Cazorla
alipata mpira ndani ya 18 ya Westbrom. Jonas Olsson, beki wa Westbrom alienda kumkaba Cazorla.
Olsson alijaribu kupiga mpira, lakini, Cazorla aliupeleka mpira kushoto, Olsson
aliukosa mpira na ilionekana kama Olsson aliupiga mguu wa kulia wa Cazorla.
Cazorla alianguka na Arsenal walipata penalti.
Marudio
yalionyesha kwamba Olsson aliukosa mpira, lakini, pia marudio yalionyesha
kwamba Olsson hakugusa mguu wa Cazorla na Cazorla alianguka bila kuguswa.
Inasikitisha
kwamba mchezaji mzuri kama Cazorla anajiangusha makusudi ili timu yake ipate
penalti. Katika mpira kwa sasa timu inaweza kushinda mechi kwa sababu mchezaji
wao anajiangusha ndani ya 18 na refa anaamua ipigwe penalti.
Msimu huu FA
kwa kweli wamejaribu kuwapunguza wachezaji wanaojiangusha katika ligi ya
Uingereza. Msomaji utakuwa unajua, kwamba wachezaji wengi katika ligi ya
Uingereza msimu huu wamepata kadi ya njano kwa sababu wamejiangusha.
Mara nyingi
katika ligi ya Uingereza marefa wamefanya
vizuri kuwapa kadi za njano wachezaji wanaojiangusha. Lakini, mara kwa mara, na hasa katika msimu huu, marefa wamekosea na
wametoa kadi ya njano kwa wachezaji ambao kweli wamechezewa faulo na hawakujiangusha. Kwa mfano, Torres alipata kadi njano ya pili katika mechi
dhidi ya Manchester United msimu huu. Lakini, marudio yalionyesha kwamba Torres
kweli alichezewa faulo na Johny Evans.
Marefa wengine
pia wamefanya kosa la kuwapa mipira ya adhabu kuelekea timu za upinzani wachezaji ambao wamejiangusha kwa makusudi.
Mwezi huu fainali za Kombe la Dunia la vilabu zinafanyika nchini Japan.
Na kwa mara
ya kwanza katika historia ya mpira wa miguu ‘Goal line technology’- teknolojia
ya mstari wa goli itatumiwa. Bado hatuna
teknolojia ambayo inaweza kuona kama mchezaji amejiangusha kwa makusudi. Lakini, mimi nafikiri , kama mchezaji anajiangusha
ndani ya 18 au nje ya 18, na refa anampa penalti au faulo, na marudio yanaonyesha
kwamba mchezaji huyo kweli alijiangusha, basi, nafikiri mechi ikiisha , mchezaji huyo angepata kadi
nyekundu na angefungiwa mechi 3.
Kama
mchezaji anamwambia mchezaji mwingine neno la kibaguzi katika mechi, na refa haoni, mchezaji huyo bado atafungiwa
mechi kadha kama timu ya upinzani inawasilisha rasmi malalamiko. Kwa mfano,
msimu uliopita Suarez alimwambia Evra neno la kibaguzi katika mechi dhidi ya
Man U katika FA cup. Mechi ilipoisha,
Evra alilalamika rasmi, na marudio yalionyesha kwamba Suarez kweli
alimwambia Evra neno la kibaguzi. Suarez alifungiwa mechi 8.
Naamini
kwamba kama wachezaji wangepata kadi nyekundu kama wanajiangusha makusudi , na kama
wanaweza kufungiwa hata kama refa hajaona, lakini, marudio yameonyesha kwamba wamejiangusha,
basi,
wachezaji wachache sana wangeendelea na tabia huyo ya kujiangusha
makusudi.
Post a Comment