Wananchi wa eneo la M.R mjini Iringa wakitazama mtoto aliyetupwa kwenye Dampo leo(picha na Patrick Tenywa) |
Mwili wa mtoto aliyetupwa huu ukiwa ndani ya dampo (tunaomba radhi kwa picha hizi) |
Hapa msamaria mwema akiufunua mwili huo uliotupwa katika dampo ukiwa katika mfuko wa rambo |
Askari polisi wakiupatika mwili huo katika Taxi kuupeleka chumba cha maiti Hospitali ya mkoa wa Iringa |
ZIKIWA zimepita siku
takribani tano toka kukutwe kwa mwili wa mtoto mchanga katika eneo la
Semtema jirani na makazi ya wanafunzi wa chuo kimoja cha dini
mkoani Iringa ,simanzi na majonzi zimeendelea kutanda katika manispaa
ya Iringa baada ya mtoto mwingine kutupwa katika dampo la taka katika
eneo la stendi ya M.R mjini Iringa.
Wakizungumzia matukio hayo ya wanawake kufanya vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto wanaowazaa baadhi ya wanawake mjini Iringa wamelitaka jeshi la polisi na jamii nzima kusaidiana kuendesha misako mikali dhidi ya wanawake wanaofanya vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya watoto wao.
Sarah Sanga mkazi wa Miyomboni alisema kuwa matukio ya wanawake kutoa mimba na kutoa watoto yameendelea kuwa ni tishio katika Manispaa ya Iringa na kuwa iwapo jeshi la polisi halitafanya uchunguzi wa kina na kuwabaini wanawake wanaofanya vitendo hivyo vya ukatili yawezekana matukio hayo yakaendelea kutikisa katika mji wa Iringa.
Sanga alisema kuwa awali mji wa Iringa ulikuwa ukiongoza kwa matukio kasi ya maambukizi ya VVU ila kwa sasa matukio yanayotishia zaidi ni ya wanawake kutoogopa janga la UKIMWI na kuendelea kushika mimba ovyo na baada ya kubakiza miezi michache ya kuzaa wamekuwa wakifanya ukatili kwa kutoa mimba hiyo.
" Hivi hawa wanawake wanaoshika mimba na kutupa watoto kwanini wanafanya mapenzi bila kinga ...sasa leo mimba wametoa na kutupa mtoto na kama wameambukizwa UKIMWI nao watautoa na kuutupa ....dawa ni kulea mimba na kuzaa salama bila kufanya ukatili huu"
Alisema yawezekana sababu ya wanawake hao kutoa mimba ikawa ni wanaume wanawa wapo mimba hiyo kuonyesha dalili ya kuikataa na ndio sababu ya kukimbilia kutoa baada ya kukataliwa ila yawezekana pia wanaohusika na utoaji mimba hiyo ni wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wamekuwa wakiishi maeneo ya jirani na maiti hizo za vichanga vinapokutwa zikiwa zimetupwa.
Huku Said Ally akishauri wanawake kuwafichua wanawake wenzao ambao siku za karibuni walionekana na mimba na ghafla mimba hizo kutoweka kwani iwapo wanawake watatoa ushirikiano kwa kuwafichua wanaofanya hivyo vitendo hivyo vya kinyama vitapungua .
"Ujue hapa ambapo mwili huu wa mtoto umeokotwa katika dampo kuna Grosary kama mbili zinazozunguka dampo hili ila pia ni jirani kabisa la eneo la vibanda vya UVCCM maarufu kama vibanda vya kitimoto mjini Iringa hivyo waliotupa mtoto huyo ni wanaotumia dampo hili na uwezekano wa kuwakamata wahusika ni mkubwa zaidi kwa kupiga kura za siri "
Akizungumzia juu ya mwili huo wa mtoto wa kike uliokutwa katika dampo hilo la M.R wananchi hao walisema kuwa mwili wa mtoto huyo ambae anakadiriwa kubakiza kama wiki mbili ama moja ili azaliwe inadaiwa wahusika wa tukio hilo ni wenyeji wa eneo hilo .
Mkuu wa wilaya ya Iringa Dr. Leticia Warioba aliwataka mabinti na vijana wilayani hapo kuepuka kukimbilia kushika mimba wala kupeana mimba bila kuwa na uhakika wa ndoa.
Hata hivyo alisema serikali ya wilaya itaendelea kutoa elimu zaidi kwa vijana ili kupunguza tatizo la watoto kutupwa katika wilaya ya Iringa .
Wakizungumzia matukio hayo ya wanawake kufanya vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto wanaowazaa baadhi ya wanawake mjini Iringa wamelitaka jeshi la polisi na jamii nzima kusaidiana kuendesha misako mikali dhidi ya wanawake wanaofanya vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya watoto wao.
Sarah Sanga mkazi wa Miyomboni alisema kuwa matukio ya wanawake kutoa mimba na kutoa watoto yameendelea kuwa ni tishio katika Manispaa ya Iringa na kuwa iwapo jeshi la polisi halitafanya uchunguzi wa kina na kuwabaini wanawake wanaofanya vitendo hivyo vya ukatili yawezekana matukio hayo yakaendelea kutikisa katika mji wa Iringa.
Sanga alisema kuwa awali mji wa Iringa ulikuwa ukiongoza kwa matukio kasi ya maambukizi ya VVU ila kwa sasa matukio yanayotishia zaidi ni ya wanawake kutoogopa janga la UKIMWI na kuendelea kushika mimba ovyo na baada ya kubakiza miezi michache ya kuzaa wamekuwa wakifanya ukatili kwa kutoa mimba hiyo.
" Hivi hawa wanawake wanaoshika mimba na kutupa watoto kwanini wanafanya mapenzi bila kinga ...sasa leo mimba wametoa na kutupa mtoto na kama wameambukizwa UKIMWI nao watautoa na kuutupa ....dawa ni kulea mimba na kuzaa salama bila kufanya ukatili huu"
Alisema yawezekana sababu ya wanawake hao kutoa mimba ikawa ni wanaume wanawa wapo mimba hiyo kuonyesha dalili ya kuikataa na ndio sababu ya kukimbilia kutoa baada ya kukataliwa ila yawezekana pia wanaohusika na utoaji mimba hiyo ni wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wamekuwa wakiishi maeneo ya jirani na maiti hizo za vichanga vinapokutwa zikiwa zimetupwa.
Huku Said Ally akishauri wanawake kuwafichua wanawake wenzao ambao siku za karibuni walionekana na mimba na ghafla mimba hizo kutoweka kwani iwapo wanawake watatoa ushirikiano kwa kuwafichua wanaofanya hivyo vitendo hivyo vya kinyama vitapungua .
"Ujue hapa ambapo mwili huu wa mtoto umeokotwa katika dampo kuna Grosary kama mbili zinazozunguka dampo hili ila pia ni jirani kabisa la eneo la vibanda vya UVCCM maarufu kama vibanda vya kitimoto mjini Iringa hivyo waliotupa mtoto huyo ni wanaotumia dampo hili na uwezekano wa kuwakamata wahusika ni mkubwa zaidi kwa kupiga kura za siri "
Akizungumzia juu ya mwili huo wa mtoto wa kike uliokutwa katika dampo hilo la M.R wananchi hao walisema kuwa mwili wa mtoto huyo ambae anakadiriwa kubakiza kama wiki mbili ama moja ili azaliwe inadaiwa wahusika wa tukio hilo ni wenyeji wa eneo hilo .
Mkuu wa wilaya ya Iringa Dr. Leticia Warioba aliwataka mabinti na vijana wilayani hapo kuepuka kukimbilia kushika mimba wala kupeana mimba bila kuwa na uhakika wa ndoa.
Hata hivyo alisema serikali ya wilaya itaendelea kutoa elimu zaidi kwa vijana ili kupunguza tatizo la watoto kutupwa katika wilaya ya Iringa .
Post a Comment