Pablo Zabaleta amefunga bao kunako dakika za mwisho mwisho na kuisaidia
Manchester City kuipiku Stoke City kwa bao moja kwa bila na kufuzu kwa raundi ya
tano ya michuano ya kuwania kombe la FA.
Manchester City haikutumia nafasi walizopata kufunga wakati wa mechi
hiyo.
Juhudi za washambuliaji wake David Silva na Carloz Tevez hazikufua dafu pale mikwaju yao ilipogonga mlingoti.
Juhudi za washambuliaji wake David Silva na Carloz Tevez hazikufua dafu pale mikwaju yao ilipogonga mlingoti.
Kipa wa Stoke Thomas Sorenson vile vile alifanya kazi ya ziada kuokoa mikwaju
ya washambuliaji hao wa Manchester City.
Stoke haikufanya mashambulizi yoyote ya maana wakati wa mechi hiyo.
Lakini wakati mechi hiyo ilipoonekana kuisha kwa timu hizo mbili kutoshana
nguvu, Sergio Aguero alimpa pasi nzuri Zabaleta ambaye aliiweka kimyani na
kuwaacha mashabiki wa Stoke vinywa wazi.
Mchezaji wa ziada ya Stoke Cameron Jerome, alipata nafasi nzuri sana ya
kusawazisha lakini, akaupiga mpira ovyo licha ya kuwa katika nafasi nzuri na
kipa pekee.
Ushindi huo ni wa kwanza kwa Manchester City katika uwanja huo wa Stoke tangu
mwaka wa 1999, wakati timu hizo mbili zilikuwa zinacheza ligi daraja ya
pili.
Bbc/swahili
Post a Comment