MH. ZITTO KABWE AWEKA WAZI KUHUSU KUGOMBEA URAIS

Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh. Zitto Kabwe ameamua kuweka wazi kuhusu kugombea uraisi mwaka 2015, alifunguka kwa kusema,

"Ngoja niweke wazi kabisa. Ninaulizwa sana kuhusu suala la Urais 2015 baada ya kauli za wanachama waandamizi wa CHADEMA kunukuliwa kuzungumzia suala hilo. Jibu langu kwa wote wenye kutaka kusikia kauli yangu ni kwamba 'katika moja ya maazimio yangu ya mwaka mpya 2013 ni kutoongelea kabisa suala la Urais 2015. Hivyo sitaongelea suala hili. Sitasema kitu kuhusu suala hili mpaka baada ya Katiba mpya kupatikana na chama changu kuweka utaratibu na mchakato wake'.

Post a Comment

Previous Post Next Post