Kwa kile kinachoonekana kushindikana kwa suluhu
juu ya mgogoro wa gesi, hali inaonekana kuwa bado ni tete mbali na jitihada za
Waziri Mkuu kuja kutatua mgogoro hou. Baada ya taarifa yake ya majumuisho
aliyoitoa juzi jioni hapa Mtwara inaonekana bado kuacha maswali mengi miongoni
mwa Wananchi. Hali asubuhi ya jana imekuwa ni tofauti kidogo kulinganisha na juzi.
Jana kila unapopita majadiliano na mazungumzo yao ni juu ya hotuba ya juzi ya
majumuisho juu ya hoja za mgogoro wa gesi. Inaonekana watu bado wanamashaka na
msimamo wa serikali.
Nimebahatika kuongea na wananchi wachache juu
ya jambo hili lakini wote wameonekana kutosadiki msimamo wa Serikali kwa kile
wanachodai ni propaganda za kisiasa na uhalisia wa mambo.
Wakisisitiza katika hili walihoji; “Hivi wewe
ndugu yangu, kama msimamo wa serikali ilikuwa ni kusafirisha gesi
iliyosafishwa, je kipi kilkistahili kuanza kujengwa kati ya kiwanda cha
kusafisha na bomba la kusafirishia gesi?”
Mwingine akahoji; “Unawezaje kukubali
kusafirisha umeme kupelekwa Songea ambako ni mbali na kushindwa kupelekwa Dar
es salaam ambako ni karibu? Wapi kutakuwa na gharama kubwa zaidi? Tunajuwa
janja yao ilipo kwa hiyo, msimamo wetu uko palepale kwamba kama shida yao ni
umeme basi usafirishaji wa gesi kwa bomba haiwezekani. Ni kipi kinachowafanya
kung’ang’ania usafirishaji huo kama si wizi?”
Kwa hakika inaonekana bado kuna jambo serikali
inapaswa ilifanye zaidi ya hiki kinachoaminika ni suluhu inayotangazwa tangu juzi,
kwani nadhani bado suluhu hiyo haijaingia masikioni mwa watu. Mikanganyiko ni
mingi, wengi wanahoji pia juu ya sababu hasa ya Waziri Mkuu na jopu lake kubwa
kuja huku; je ilikuwa ni kusikiliza hoja na misimamo ya Wanakusini au kutoa
msimamo wa Serikali kwamba lazima gesi isafirishwe kwa bomba? Bado hoja ni
nyingi kwa kweli.
Wananchi wamekwenda mbali zaidi na kuponda hoja
kuhusu kuchelewa kumalizika kwa ujenzi wa barabara, maeneo ya Somanga. Kwani
kwa mujibu wa Waziri Mkuu ni kwamba; barabara imechelewa kukamilika ujenzi wake
kwa sababu ya kufariki kwa Mkandarasi. Hoja hii inapingwa kwa kuhoji kipindi
tangu barabara hiyo ilipoanza kujengwa na kifo cha Mkandarasi huyo, kwamba
hakuna uhusiano wowote. Wanatole mfano hapa kwamba itawezekanaje msiba ushindwe
kumaliza ujenzi wa barabara kipande cha Kilometa 60 ndani ya zaidi ya miaka
kumi?
Ni wazi kabisa kwamba, mbali ya taarifa
zinazotolewa juu ya kumalizika kwa mgogoro huu lakini ukweli ni kwamba hali
bado ni tete na kunahitajika busara zaidi kutafakari jambo hili zaidi ya kusimamia
misimamo ambayo itatuletea matatizo. Inatupasa tutafute suluhu ya kudumu ili
hata kile kinachotegemewa kufanywa kiweze kuleta tija kwa nchi yetu na si
machafuko.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Wabariki
Watanzani.
Hassani Samli,
Mtwara.
+255717340671
Post a Comment