Mkurugenzi wa Ludewa Fidelis Lumato
Sherehe za kuwaaga na kuwakaribisha watumishi wa Halmashauri ya
wilaya ya Ludewa zafana usiku huu katika ukumbi wa Halmashauri ya
wilaya ya Ludewa .
Katika sherehe hizo ambazo pia zimeambatana na kuuaga mwaka 2012 na
kuukaribisha mwaka 2013 zinafanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya
Ludewa huku viongozi mbali mbali wa Wilaya na Halmashauri hiyo ya
wilaya ya Ludewa wakiwa wamepamba sherehe hiyo.
Akizungumza
katika sherehe hiyo mratibu wa kamati ya maandalizi ya sherehe hiyo
Gladness Mwano amesema kuwa katika sherehe hiyo jumla ya watumishi
6 wanaagwa rasmi baada ya kustaafu na watumishi 14 wanahama huku
watumishi 5 wakikaribishwa katika Halmashauri hiyo ya wilaya ya
Ludewa .
Watumishi wanaostaafu katika Halmashauri hiyo
ni pamoja na Augusta Kayombo ( Idara ya afya), Gerold Kayombo ( katibu
TSD), Ignas Mkechi (ukaguzi wa shule), Beneth Nzalamoto ( Idara ya
afya) , Edwird Masangula (idara ya fedha) na Ireen Mtetemela ( idara ya
utawala).
Wakati watumishi waliohama ni pamoja na
aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Hilda Lauwo
aliyehamia Maswa , Juma ,Ally (afisa utumishi na utawala aliyehamia
Mbinga, Advery Dallu Afisa utumishi na utawala amehamia TAMISEMI
Dodoma, Alto Liwolelu (Mwanasheria aliyehamia Kilolo), Emmanuel
Mlelwa (afisa elimu sekondari aliyekwenda Pangani ,Christopher
Nyandiga (mhandisi aliyehamia RAS Njombe), Rashid Mtamila ( Mhandisi wa
ujenzi aliyehamia Sumbawanga),Gumbo Mvanda ( afisa misitu anahamia Ras
Njombe),Daud Kumburu (afisa ufugaji nyuki anahamia Ras Njombe ), Mussa
Sechonge (Afisa kilimo wadudu anakwenda Morogoro),Rose Lutambi
(muunguzi mifumo ya kompyuta anakwenda Njombe mji) na Mariam
Kinyamagoha (afisa muuguzi anahamia Mufindi).
Aidha
Halmashauri ya wilaya ya Ludewa imepokea watumishi wapya ambao
wanachukua nafasi ya waliohama na kustaafu ikiwemo nafasi ya
mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo inayochukuliwa na Fidelis
Lumato aliyehamia kutoka Tarime, Mathan Chalamila (mwanasheria
anayehamia kutoka Njombe DC ,Maternus Ndumbaro (afisa elimu sekondari
anayehamia kutoka Makete , Baraka Mkuya (mahandisi ujenzi anayehamia
kutoka Sumbawanga MC na Antony Mbi
nda (katibu TSD anayehamia kutoka
Mufindi)
Akizungumza katika sherehe hiyo mwenyekiti wa
Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mateo Kongo alisema kuwa Halmashauri
hiyo imefarijika kwa utendaji wa watumishi waliopita na kuwakaribisha
wapya huku akiahidi kuwapa ushirikiano zaidi.
|
Post a Comment