Uwanja wa ndege wa Gao wakombolewa

Wizara ya Ulinzi ya Ufaransa inasema kuwa jeshi linaloongozwa na Wafaransa limeuteka uwanja wa ndege wa mji wa Gao, ngome ya wapiganaji ya Kiislamu kaskazini mwa Mali.

Daraja muhimu pia wameliteka.
Mapigano yanaendelea.
Gao ni mmoja kati ya miji mikuu mitatu ya kaskazini mwa Mali iliyotekwa na wapiganaji mwaka jana.
Siku ya Ijumaa wanajeshi wa Mali na Ufaransa waliukomboa mji wa Hombor kilomita 160 kutoka Gao.
Umoja wa Afrika umesema unataka kuzidisha idadi ya wanajeshi wa kuweka amani nchini Mali, na imeomba nchi zanachama kujitolea kwa wanajeshi zaidi katika wiki zijazo.
Piya umeuomba Umoja wa Mataifa usaidie kuwasafirisha wanajeshi hao hadi Mali.

Post a Comment

Previous Post Next Post