Mkuu wa wilaya ya Kilwa Abdallah Ulega, (kushoto) akishuhudia zoezi la utiaji wa sahihi wa mkataba huo wa miaka mitatu kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, Addo Mapunda akitiliana saini na Mratibu wa Mradi wa mpango wa ufundishwaji wa Lugha ya Kingereza kwa njia ya teknorojia ya kisasa (Techonoroji Enhanced Edcation) TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni ya Pan African Energy,inayojishughulisha na kazi ya uchimbaji,usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo Bi Anne Devilliers, wakati wa hafla hiyo fupi ya kutiliana saini iliyofanyika leo. |
Makabidhiano.
Na Abdulaziz Video,Lindi
JUMLA ya wanafunzi wapatao 1,580 wanaosoma Shule tisa za Sekondari,wilayani Kilwa, mkoani Lindi,watanufaika na mpango wa ufundishwaji wa Lugha ya Kingereza kwa njia ya teknolojia ya kisasa TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni ya Pan African Energy,inayojishughulisha na kazi ya uchimbaji,usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo.
Mradi huo wa miaka
mitatu,utagharimu jumla ya Sh, 144,945,218/-zitakazotumika kujenga
misingi bora ya Lugha ya kingereza kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza
kuanzia mwaka 2013. Hayo yameelezwa na mkurugenzi mtendaji wa
Halmashauri ya wilaya hiyo, Adoh Mapunda,alipokuwa akitoa taarifa katika
hafla fupi ya kutiliana
na saini ya utekelezaji wa mpango huo.
Mapunda alisema mpango
huo,utakaochukuwa takribani muda wa kipindi cha miaka mitatu,umeanza
rasmi mwezi huu kwa wanafunzi wapatao 1,580 wa kidato cha kwanza kutoka
Shule tisa za Sekondari zilizopo katika
wilaya hiyo.
Amezitaja Sekondari
zitakazonufaika na mpango huo kuwa ni,Kilwa day iliyopo mji mdogo wa
masoko, Mtanga, Songosongo, Mbuyuni, Kinjumbi,Miteja,Mingumbi,Kikanda na
Sekondari ya wasichana ya Ilulu.
Mkurugenzi Mapunda alisema
mafunzo hayo kwa kuanzia yatakuwa ni ya wiki sita,yameanza rasmi hivi
karibuni na kwamba walimu wapatao 30 wakiwemo (12) wa kigeni
(Volunteers) wakiwemo na walimu wazawa (18).
“Hizi Shule tisa kila moja
italazimika kutoa walimu wawili watakaopatiwa mafunzo kwa ajili ya
kuendesha mpango huu katika Shule zote hizo”Alisema Mapunda.
Aidha, Mapunda alisema kupitia
ufadhili wa mpango huo wa mafunzo ya kingereza,Halmashauri ya wilaya
itaendesha semina/warsha kutoa stadi za kufundishia masomo hayo kwa
Sekondari hizo tisa zenye walimu
wapatao (71).
Mapunda alisema mafunzo hayo
ni nyongeza kwa walimu wote waliopo katika Shule hizo tisa za mafunzo ya
kingereza ya aina mbili,TEE-TZ itakayoendeshwa kwa ufadhili wa ubalozi
wa Marekani,(RELO-Regional
English Language Office kwa Sh,24,158,480/-.
Katika ufadhili wa mafunzo hayo ya TEE-TZ na RELO jumla ya Sh,169,103,698/-ndizo zitakazotumika kwa ajili ya utekelezaji wake.
Mratibu wa mradi huo,kutoka
kampuni hiyo ya Pan African Energy,Anne Devilliers,amesema lengo la
mpango huo ni,kutaka kuwawezesha wanafunzi waelewe masomo yao kwa elimu
ya Sekondari na kuongeza viwango vya
ufaulu katika mitihani yao ya kidato cha nne.
Devilliers akasema imebainika
kwamba wapo wanafunzi waliowengi wamekuwa hawafanyi vizuri katika masomo
na mitihani yao,kutokana na kutoielewa vyema Lugha ya Kingereza.
Mkuu wa wilaya hiyo ya Kilwa,
Abdallah Ulega, ameipongeza kampuni ya Pan African Energy,na akasema
kwamba kwa kiasi furani itasaidia kuboresha kiwango cha elimu ndani ya
wilaya hiyo,mkoa na Taifa kwa ujumla.
Mpango huo,ulianza kwa
majaribio katika wilaya ya Mafia mkoani Pwani,mwaka 2010 na 2011,baada
ya kuona mafanikio yake,ndipo uongozi wa wilaya ya Kilwa,ukaamua mpango
huo kupelekwa ndani ya wilaya yao.
Post a Comment