
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Joyce
Ndalichako akionyesha karatasi ya majibu ya mmoja wa watahiniwa wa
mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2012, Dar es Salaam jana. Picha na
Edwin Mjwahuzi
--
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inaweza kukumbwa na kashfa
kubwa kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne ya 2012
yaliyotangazwa juzi na Waziri wake, Dk Shukuru Kawambwa.
Kashfa hiyo inatokana na aina ya majibu yaliyoandikwa na baadhi ya watahiniwa katika mitihani hiyo, huku wengine wakikusanya vitabu vya majibu bila kujibu chochote, hali inayohusishwa na uhaba mkubwa wa walimu katika baadhi ya shule za sekondari nchini.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Joyce Ndalichako alisema wasahihishaji walikutana na mambo ya ajabu yakiwamo matusi, michoro ya vitu visivyoeleweka, mashairi na nyimbo za muziki wa kizazi kipya (bongo fleva).Kwa habari zaidi Bofya Hapa na Endelea........>>>
Post a Comment