Bayern
Munich, wameshinda taji lao la 23 la Ligi ya soka Ujerumani –
Bundesliga na kuweka rekodi ya kuwa washindi wa mapema kabisa wa Ligi
kuwahi kushuhudiwa Ujerumani zikiwa zimesalia mechi sita msimu
kukamilikaSasa Bayern wamesalia na mechi sita wakiandaa kulionyesha taji la Bundesliga, baada ya kiungo Bastian Schweinsteiger kufunga bao la kiustadi kwa njia ya kisigino na kuwapa ushindi wa goli moja kwa sifuri dhidi ya Eintracht Frankfurt.
Vijana hao wa Mkufunzi Jupp Heynckes wamemaliza uongozi wa miaka miwili wa Borussia Dortmund kwa kushinda taji la 22 la Bundesliga mapema kuliko klabu nyingine yoyote katika historia ya miaka 50 ya ligi hiyo. Bayern walikosa nafasi baada ya Xherdan Shaqiri kuupiga mlingoti wa goli, wakati David Alaba akikosa kufunga mkwaju wa penalti. Ushindi huo uliwapa Bayern uongozi wa jumla ya pointi 75
Jupp Heynckes amesema ni vizuri sana kushinda tena taji baada ya miaka 23. aliwaongoza Bayern kutwa mataji ya mwaka wa 1989 na 1990 wakati akiwa kocha. Heynckes atampisha Mhispania Pep Guardiola mwishoni mwa msimu huu wakati ambapo Bayern huenda watakuwa wameongeza mataji mengine mawili, Champions League na Kombe la Shirikisho. Nahodha wa Bayern Philip Lahm anasema sasa wameangazia macho yao katika mchuwano wa marudiano wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Juventus.
Post a Comment