‘Bado nipo nipo sana, sioni mwanamke wa kuoa’ - Timbulo

TIMBULO
Hitmaker wa Samson na Delilah, Timbulo ambaye yupo mbioni kuachia video ya ‘Sina Makosa’ wiki ijayo, amesema yeye ni mwanachama mkubwa wa kambi ya MwanaFA kwakuwa bado yupo yupo sana. Amesema hana mpango tena wa kuoa na isahaulike kabisa baada ya kuona kuwa wanawake wengi wanampenda kwakuwa ni msanii na hawana mapenzi ya dhati.
Timbulo amesema hayo baada ya kuwaahidi mashabiki wake kwamba anakaribia kuoa ila kwa sasa amebadilisha mawazo baada ya uhusiano wake kumwendea ndivyo sivyo na kumkata mudi na matarajio ya kufunga ndoa.
Ameiambia Hisia za Mwananchi kuwa msichana aliyekuwa amepanga amfanye mke amemzingua vibaya.
“Sahau kuhusu mimi kuoa, muolewaji hakuna bana, kwa wastani wa maisha ya furaha ya siku 1 kwa sita, zilizobaki kwenye week ni ugomvi, huzuni na kutoelewana siwezi, nitakufa na pressure,” amesema.

Post a Comment

Previous Post Next Post