Hawa ni baadhi ya wasimamizi wa kura za uchaguzi mdogo wa udiwani kata Temi jijini Arusha.
LEO
tarehe 14 July 2013 ni siku ya kihistoria katika jiji la Arush kwa kuwa
ndio siku niliyokua ikisubiriwa na watu wengi ili kuona ni kitu gani
kitakachojiri katika zoezi zima la uchaguzi mdogo wa madiwani katika
kata nne za Arusha mjini.
Na
kwa mujibu wa repoters wa mtandao huu wa kinng Jofa Blog ni kwamba
CHADEMA wameibuka kidedea kwa kuweza kushinda katika uchaguzi huo mdogo
wa madiwani katika kata zote nne. Ambapo awali uchaguzi huo uliingia
dosari baada ya shambulio la bomu lililorushwa katika uwanja wa soweto
siku moja kabla ya uchaguzi na hatimae uchaguzi huo kuairishwa na
kufanyika leo jumapili tarehe 14 July 2013.
Uchaguzi
umefanyika ambao leo umeonekana kuwa na utulivu mkubwa na hatimaye
zoezi lakupiga kura na kuzihesabu likakamilika majira ya jioni.
Endelea kutembelea Hisia za Mwananchi kwa habari zaidi kuhusiana na uchaguzi huo wa madiwani.
Post a Comment