Drake kumshirikisha baba yake mzazi kwenye album yake "Nothing Was The Same"


Ikiwa siku za kuachia album yake "Nothing Wa The Same" zinakaribia (Sep 24), habari zaidi zinazid kutoka. Habari zilizoenea sasa ni kuwa Drake atamshirikisha baba yake mzazi kwenye ngoma ambayo itakuwa ni bonus kwenye album hiyo " Heat of the moment."

“Naishi katika ndoto za baba yangu. Baba yangu alitaka kuwa muimbaji maarufu, kulikuwa na interview zingine ambazo waliniuliza kuhusu baba yangu, na sikutaka kuongelea kuhusu hilo, na kuna ngima ambazo sijamfanya baba yangu kuonekana ni mtu mkubwa, mwisho wa siku, baba yangu anajua kuwa nampenda na kuwa ni rafiki yangu mkubwa." amesema Drake.
Bado haijawekwa wazi kama baba mzazi wa Drake, Dennis Graham ataimba kwenye ngoma hiyo au sauti yake tu ndio itakayoskika kama sample, kama kwenye ngoma ya zamani ya Drake “Jodeci Freestyle” aliyomshirikisha J. Cole.

Post a Comment

Previous Post Next Post