Jana, Agosti 28, 2013 Wamarekani waliadhimisha rasmi miaka 50 tangu
kufanyika kwa maandamano makubwa ya kudai haki sawa kwa "watu weusi"
nchini humo.
Katika maadhimisho hayo, kamera ya "swahilivilla blog" iliegeshwa kando ya lango la kuingia na kushuhudia watu maarufu nchini wakipekuliwa kwa sababu za usalama kabla ya kuingia ndani sherehe hizo ambazo zilihudhuriwa na maelfu ya watu kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Picha hizo zinaonekana hapo juu na hapa chini pamoja na sauti...
Katika maadhimisho hayo, kamera ya "swahilivilla blog" iliegeshwa kando ya lango la kuingia na kushuhudia watu maarufu nchini wakipekuliwa kwa sababu za usalama kabla ya kuingia ndani sherehe hizo ambazo zilihudhuriwa na maelfu ya watu kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Picha hizo zinaonekana hapo juu na hapa chini pamoja na sauti...
Tuliobahatika kuwanasa katika kamera ya swahilivilla muigizaji Jimmy
Foxx, pale alipotolewa ndani ya gari na maofisa kuanza kupekua gari
alilolipanda kabla ya kuingia ndani ya eneo la Lincoln Memorial
Washington DC. Picha zote na (swahilivilla.blogspot.com)
Muigizaji wa filamu Jimmy Foxx akishuhudia gari lake likipekuliwa kabla
ya kuingia ndani ya tukio la maadhimisho ya miaka 50 ya March on
Washington DC
Mwigizaji wa filamu Angelha Bassett Evelyn alipotolewa kwenye gari lake
na maofisa kuanza kulipekua kabla ya kuingia ndani ya eneo la Lincoln
Memorial Washington DC
Mshangao mkubwa watu walioupata ni pale mtoto wa Rais wa zamani nchini
Marekani John F. Kennedy, Caroline Kennedy ambae ni balozi mteule Nchini
Japani, alipoingia na Cab (Taxi). cha kuchangaza pia ni pale gari lake
lilipopekuliwa bila ya kujali ukubwa au cheo alichonacho na kufata
sheria ya upekuzi kama wengine magari yao yalivyopekuliwa.
Caroline Kennedy akiishangaa flash yaswahilivilla blog pale ilipomnasa akisubiri gari lake likifanyiwa upekuzi wa lazima
Mwigizaji maarufu wa filamu nchini Marekani Forest naye pia gari lake
lilifanyiwa upekuzi na maofisa wa usalama baada ya kuwasili katika endeo
la Sherehe za miaka 50 ya March on Washington DC
Vile vile kamera ya swahilivilla blog imemnasa Rajiv “Raj” Shah
American Economic development specialist, alipotolewa nje ya gari lake
na kufanyiwa upekuzi wa lazima siku ya Jumatano Aug 28, 2013 Washington
DC
Rajiv “Raj” Shah akishangaa kwambalii flash ya swahilivilla.blog baada
yakutolewa ndani ya gari lake na kufanyiwa utaratibu wa kupekuliwa.
Ofisa Usalama akifanya upekuzi wa magari ya watu maarufu yanayoelekea
katika maadhimisho ya miaka 50 ya March on Washington DC siku ya
jumatano Aug 28.
Mwanasheria Mkuu wa jimbo la California Kamala Harris pia alishushwa
ili kuruhusu upekuzi wa gari kabla ya kuingia katika sherehe za
maadhimisho ya miaka 50 ya March on Washington
Kamala Harris aliamua kusogea na kusalimiana na baadhi ya watu waliokua
karibu yake pamoja na kamera ya swahilivilla wakati gari yake
ikipekuliwa kabla ya kuingia katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50
ya March on Washington
Ni Oprah Gail Winfrey pekee ambaye hajatoka kwenye gari lake ambalo
lilipekuliwa na kuruhusiwa kuondoka bila ya kutolewa ndani ya gari hilo
alilokua amalipanda
Oprah Gail Winfrey akishangaa kwa mbali flash ya swahilivilla wakati
anaelekeaa ndani ya Lincoln Memorial Washington Washington DC
Chief wa swahilivilla Abou Shatry akiwa katika 50th anniversary March
on Washington DC Siku ya Jumatano 28, 2013 Rais Barak Obama, leo ametoa
changamoto kwa kizazi kilichopo kuwaenzi mashujaa walioandamana mwaka
1963 kudai haki sawa kwa watu wa rangi zote nchini Marekani. JAMII RADIO
ina ripoti kamili. Sikiliza. Na pia kwa taswira zaidi bofya hapa
Post a Comment