RIPOTI MAALUM YA MASHAMBULIZI YA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA HII HAPA




BW.SAED  KUBENEA MKURUGENZI  WA GAZETI LA MWANAHALISI
..........................................................................................................................................................................................................
 
Ongezeko katika mashambulizi yaliyopo dhidi ya sehemu ya sheria kandamizi, na udhibiti wa muda mrefu wa gazeti moja la kukosoa unachangia hofu na udhibiti binafsi miongoni mwa waandishi wa habari nchini Tanzania, Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari ilisema katika ripoti mpya iliyotolewa leo. 

Licha ya sifa nzuri ya Tanzania ya uwazi na demokrosia, wananchi wayo wananyimwa taarifa muhimu.

"Mashambulizi ya hivi majuzi ya waandishi wa habari, pamoja na sheria zinazopinga vyombo vya habari, zinawafanyya maripota kuhofia zaidi usalama wao," alisema Tom Rhodes, mshauri na mwandishi wa ripoti wa CPJ Afrika Mashariki. "Udhibiti wa binafsi una maana ya kutoridhishwa kusikorekodiwa." 

Ripoti, inayoitwa "Shida Isiyoonekana ya Vyombo vya Habari vya Tanzania," inataja mwiba katika mashambulizi na vitisho kama hivyo mwaka uliopita
-CPJ imeweka kumbukumbu 10 za miezi 11 iliyopita-ikiwa ni pamoja na polisi kumwua mwanakamera mkongwe alipokuwa akiangazia msafara wa upinzani


Hakuna afisa yeyote aliyewajibishwa kwa mauaji hayo ,Ripoti pia inaulizia taswira ya kimataifa ya serikali ya Tanzania kuhusu kujitolea kwa uwazi na demokrasia, ikisema kuwa angalau sheria 17 zinazohusu ukandamizaji wa vyombo vya habari zingalipo. 


Chini ya sheria hizi, gazeti moja la kukosoa, MwanaHalisi, limeondolewa kwa muda usiojulikana, hatua ambayo waandishi wengi wa habari wanaiona kama ujumbe unaotumwa kwenye mashirika yote ya vyombo vya habari.


Serikali imeahidi kurekebisha sheria za vyombo vya habari na imetia sahihi kwenye Mradi Huru wa Ushirikiano wa Serikali, juhudi za pamoja za kukuza uwazi. 

Ilhali baada ya miaka mingi ya majadiliano, haijatoa sheria ya kutekeleza ufikiaji wa taarifa au kubadilisha sheria mbalimbali zilizopo zenye vikwazo.

Kama mojawapo ya mapendekezo muhimu ya ripoti, CJP inasisitiza kuwa serikali inastahili kushauriana na vyombo vya habari na waandishi wa habari ili kutunga na kutekeleza sheria ya kufikia taarifa inayohakikisha kuwa wananchi wana ufikivu mpana wa nyaraka za umma.

 Inastahili kuondoa vipengele na sheria zote zinazonyima uhuru wa vyombo vya habari na kuondoa marufuku na kuondoshwa kwa muda kwa vyombo vya habari. Uchunguzi wa kina wa mashambulizi kwa waandishi wa habari lazima ufuatiliwe, ili wahusika washtakiwe kwa mujibu wa sheria.

"Hatua za nidhamu za serikali ya Tanzania kuhusu uhuru wa vyombo vya habari na kujieleza ni ishara tosha kuwa inahisi kutishwa tunapokaribia uchaguzi wa urais na ubunge 2015," Rhodes alisema.

 "Lakini ili kutimiza viwango vya kimataifa vya uwazi na demokrasia, lazima serikali iwaruhusu waandishi wa habari kuripoti kuhusu kile kinachoendelea nchini bila hofu ya matokeo hasi."

 IMETOLEWA  NA

CPJ ni shirika huru, lisilo la faida linalofanya kazi ili kulinda uhuru wa vyombo vy habari duniani kote.

 Nairobi, Agosti 6, 2013-

Post a Comment

Previous Post Next Post