Serikali yapokea mizinga ya Kisasa 200 ya ufugaji nyuki
Serikali
wilayani Sikonge mkoani Tabora imesema itaendelea kuhifadhi na kulinda
mazingira ya asili katika pori la akiba la Ugala kwa ajili ya shughuli za
utalii na ufugaji nyuki kwa manufaa ya wananchi wa wilaya hiyo na Taifa.
Kauli
hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Sikonge Hanifa Selengu, kwenye makabidhiano
ya mizinga mia mbili ya kisasa ya ufugaji nyuki yenye thamani ya shilingi
milioni 24 iliyotolewa na shirika lisilo la kiserikali la Friedkin Conservation
Fund (FCF) ambalo linajishughulisha katika uwindaji na utalii.
Mkuu
huyu wa wilaya amesema wananchi wanaoishi katika vijiji vinavyopakana na
mapoli ya akiba hawana budi kuendelea kuhakikisha kuwa maeneo hayo
yanahifadhiwa kikamilifu kwa manufaa yao.
Katika
hutuba yake mkuu wa wilaya ya Sikonge ameritaka shirika hilo kusaidi vifaa vya
kisasa vya ulinaji asali kwa wananchi hawa, Bw Nelson Kuwai ambae ni meneja
mahusiano na maendeleo ya jamii wa shirika la Friedkin Conservation Fund
amesema wanaowajibu wa kusaidi vifaa hivyo kama ambavyo wamekuwa wakichangia
miradi mingine ya maendeleo.
Awali
akisoma taarifa mwana kikundi Cha Vikoba tumo Edward Joseph amesema kikundi
hicho cha kuweka na kukopa kinakabiliwa na changamoto mabali mbali za kiuchumi
ikiwa pamoja na ukosefu wa elimu ya ujasiliamali.
Pamoja na shuhguli za uhifadhi shirika la Friedkin Conservation Fund na washirika wake wamekuwa wa kichaingia shughuli za maendeleo za vijiji ambavyo vinapakana na poli la akiba la ugala ili kuboresha maisha ya wananchi hao.
Post a Comment