ANUSURIKA KUPOKEA KICHAPO KITAKATIFU MARA BAADA YA KUOKOLEWA NA WASAMARIA WEMA WAKATI AKIJARIBU KUTAPELI KATIKA UZINDUZI WA FILAMU YA LULU MWISHONI MWA WIKI


 
Tapeli (katikati) akiwa anatolewa nje ya Ukumbi wa Mlimani City wakati wa uzinduzi wa Filamu ya Elizabeth Michael aka LULU mara baada ya kukamatwa akijaribu kutapeli katika moja ya Baa iliyokuwa ikitoa huduma kwa wakazi wa jiji waliofika kwaajili ya Kutazama uzinduzi wa Filamu ya Lulu mwishoni mwa wiki
 Kijana ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja (katikati) akiwa amebebwa mzobemzobe na baadhi ya wafanyakazi wa Baa iliyokuwa ikitoa huduma ndani ya Ukumbi wa Mlimani city mara baada ya kukamatwa akitaka kufanya utapeli ndani ya baa hiyo iliyokuwa ikihudumia watu mbalimbali waliofika katika Ukumbi wa Mlimani City kwaajili ya Kushuhudia Uzinduzi wa Filamu ya Lulu iitwayo FOOLISH AGE uzinduzi uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Mwishoni Mwa wiki
 Baadhi ya Wafanyakazi na walinzi wakijaribu kumnusuru kijana huyo asipokee kichapo kutoka kwa wakazi wa jiji waliofika katika uzinduzi huo, huku mmoja wa wafanyakazi wa baa hiyo akitaka kupewa maelezo juu ya tukio zima ambalo kijana huyo alipokuwa akitaka kutapeli
 Hapa sasa malezo yakiendelea huku akiwa kakamatwa haswa ili asiweze kuwachoropoka
Baadhi ya walinzi waliokuwepo katika uzinduzi huo wakiwa makini kuhakikisha amani inaendelea kuwepo na mtuhumiwa huyo anafikishwa kwenye ombo husika.Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

Post a Comment

Previous Post Next Post